< Ayubu 36 >
1 Elihu akaendelea kusema:
Elihu [finished by] saying this:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
“[Job, ] be patient with me a little longer, because I have something else to teach you. I have something else to say that God [wants you to know].
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
I will tell you what I have learned from many sources, in order to show that God, my creator, is just/fair.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
I am not saying anything to you that is false; I, who am standing in front of you, am someone who understands things (very well/perfectly) [HYP].
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
“Hey, God is [very] powerful, and he does not despise anyone, and he understands everything.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
He does not allow wicked people to remain alive, and he always acts justly toward those who are poor.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
He always watches over [MTY] those who are righteous; he allows them to sit on thrones [and rule] with kings, and they are honored forever.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
But if people [who commit crimes] are caught, they [are thrown into prison and] are caused to suffer by being fastened with chains.
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
When that happens, God shows them what they have done; he shows them the sins that they have committed, and he shows them that they have been proud/arrogant.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
He causes them to listen [MTY] to what he is warning them, and he commands them to turn away from [doing what is] evil.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
If they (listen to/heed) him and serve him, [after they get out of prison] they will prosper for all the years that they are alive and be peaceful/happy.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
But if they do not (listen/pay attention) to him, they will die violently, not knowing [why God is causing them to die].
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
“Godless/Wicked people continue being angry, and they do not cry out for help, [even] when God is punishing them.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
They die while they are still young, disgraced because of their very immoral behavior [EUP].
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
But God teaches people by causing them to suffer; by afflicting them, he causes them to listen to [MTY] what he is telling them.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
“And Job, [I think that] God [wants to] bring you out of your troubles and allow you to live without distress; he wants your table to be full of very nice food.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
But now, you are being punished [MTY] as wicked people are punished; [God] [PRS] has been punishing you (justly/as you deserve).
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
So be careful that you are not deceived by [desiring to acquire] money or that you are not ruined by [accepting] large bribes.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
[If you are deceived by those things, ] it certainly will not [RHQ] help you to cry out when you are distressed; all of your strength will not help you.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Do not wish that it would be nighttime [in order that God will not see you and punish you], because night is the time when [even] people-groups are destroyed!
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Be careful not to [begin doing] evil things, because [God] has caused you to suffer to prevent you from doing evil.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
“Hey, God is extremely powerful; there is certainly [RHQ] no teacher who teaches like he does.
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
No one has [RHQ] told him what he should do, and no one has [RHQ] said to him, ‘You have done what is wrong!’
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
People have [always] sung to praise him, so you also should never forget to praise him for what he has done.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Everyone has seen [what he has done], but [sometimes] we can see it only from far away.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
“Hey, God is very great, and we are not able to know how great he is, and we do not know how old he is.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
He draws water up [from the earth and puts it in clouds] and causes it to become rain.
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
The rain pours down from the sky/clouds; God causes abundant showers to fall on everyone.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
No one can [RHQ] understand how the clouds move [across the sky] or how it thunders in the sky where God lives.
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
He causes lightning to flash all around him, but he causes the bottom of the oceans to remain dark.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
By providing plenty of rain for us, he enables us to have abundant food.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
[It is as though] he holds the lightning in his hands, and [then] he commands it to strike where he wants it to.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
When we hear his thunder, we know that there will be a storm, and the cattle know it, too.”