< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Elihu also proceeded, and said:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Bear with me a little while, that I may show thee! For I have yet words in behalf of God.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
I will bring my knowledge from afar, And assert the justice of my Maker.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Truly my words shall not be false: A man of sound knowledge is before thee.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Behold, God is great, but despiseth not any; Great is he in strength of understanding.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
He suffereth not the wicked to prosper, But rendereth justice to the oppressed.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
He withdraweth not his eyes from the righteous; But establisheth them for ever with kings on the throne, That they may be exalted.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
And if they be bound in fetters, And holden in the cords of affliction,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
Then showeth he them their deeds, And how they have set him at defiance by their transgressions;
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
He also openeth their ears to admonition, And commandeth them to return from iniquity.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
If they obey and serve him, They spend their days in prosperity, And their years in pleasures.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
But if they obey not, they perish by the sword; They die in their own folly.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
The corrupt in heart treasure up wrath; They cry not to God, when he bindeth them.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
They die in their youth; They close their lives with the unclean.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
But he delivereth the poor in their distress; He openeth their ears in affliction.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
He will bring thee also from the jaws of distress To a broad place, where is no straitness; And the provision of thy table shall be full of fatness.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
But if thou art full of the judgment of the wicked, Judgment and justice shall take hold of thee.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
For if wrath be with him, beware lest he take thee away by his stroke, So that a great ransom shall not save thee!
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Will he esteem thy riches? No! neither thy gold, nor all the abundance of thy wealth.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Long not thou for that night To which nations are taken away from their place.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Take heed, turn not thine eyes to iniquity! For this hast thou chosen rather than affliction.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Behold, God is exalted in his power: Who is a teacher like him?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Who hath prescribed to him his way? Or who can say to him, “Thou hast done wrong”?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Forget not to magnify his work, Which men celebrate with songs.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
All mankind gaze upon it; Mortals behold it from afar.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Behold, God is great; we cannot know him, Nor search out the number of his years.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
Lo! he draweth up the drops of water, Which distil rain from his vapor;
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
The clouds pour it down, And drop it upon man in abundance.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
Who can understand the spreading of his clouds, And the rattling of his pavilion?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Behold, he spreadeth around himself his light, And he clotheth himself with the depths of the sea.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
By these he punisheth nations, And by these he giveth food in abundance.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
His hands he covereth with lightning; He giveth it commandment against an enemy.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
His thunder maketh him known; Yea, to the herds, as he ascendeth on high.

< Ayubu 36 >