< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Elihu also proceeded and sayde,
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Suffer me a litle, and I will instruct thee: for I haue yet to speake on Gods behalfe.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
I will fetche my knowledge afarre off, and will attribute righteousnes vnto my Maker.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
For truely my wordes shall not be false, and he that is perfect in knowledge, speaketh with thee.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Behold, the mighty God casteth away none that is mighty and valiant of courage.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
He mainteineth not the wicked, but he giueth iudgement to the afflicted.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
He withdraweth not his eyes from the righteous, but they are with Kings in ye throne, where he placeth them for euer: thus they are exalted.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
And if they bee bound in fetters and tyed with the cordes of affliction,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
Then will he shewe them their worke and their sinnes, because they haue bene proude.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
He openeth also their eare to discipline, and commandeth them that they returne from iniquity.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
If they obey and serue him, they shall end their dayes in prosperity, and their yeres in pleasures.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
But if they wil not obey, they shall passe by the sworde, and perish without knowledge.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
But the hypocrites of heart increase the wrath: for they call not when he bindeth them.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Their soule dyeth in youth, and their life among the whoremongers.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
He deliuereth the poore in his affliction, and openeth their eare in trouble.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Euen so woulde he haue taken thee out of the streight place into a broade place and not shut vp beneath: and that which resteth vpon thy table, had bene full of fat.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
But thou art ful of the iudgement of the wicked, though iudgement and equitie maintaine all things.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
For Gods wrath is, least hee should take that away in thine abundance: for no multitude of giftes can deliuer thee.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Wil he regard thy riches? he regardeth not golde, nor all them that excel in strength.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Be not carefull in the night, howe he destroyeth the people out of their place.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Take thou heede: looke not to iniquitie: for thou hast chosen it rather then affliction.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Beholde, God exalteth by his power: what teacher is like him?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Who hath appointed to him his way? or who can say, Thou hast done wickedly?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Remember that thou magnifie his worke, which men behold.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
All men see it, and men beholde it afarre off.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Beholde, God is excellent, and we knowe him not, neither can the nomber of his yeres bee searched out.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
When he restraineth the droppes of water, the rayne powreth down by the vapour thereof,
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
Which raine the cloudes do droppe and let fall abundantly vpon man.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
Who can know the diuisions of ye clouds and the thunders of his tabernacle?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Beholde, he spreadeth his light vpon it, and couereth the bottome of the sea.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
For thereby hee iudgeth the people, and giueth meate abundantly.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
He couereth the light with the clouds, and commandeth them to go against it.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
His companion sheweth him thereof, and there is anger in rising vp.

< Ayubu 36 >