< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Continuing in a similar manner, Eliu had this to say:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Bear with me for a little while and I will show you; for I have still more to say in favor of God.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
I will review my knowledge from the beginning, and I will prove my Maker to be just.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
For truly my words are without any falsehood and perfect knowledge will be proven to you.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
God does not abandon the powerful, for he himself is also powerful.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
But he does not save the impious, though he grants judgment to the poor.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
He will not take his eyes away from the just, and he continually establishes kings on their throne, and they are exalted.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
And, if they are in captivity, or are bound with the chains of poverty,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
he will reveal to them their works, as well as their sinfulness, in that they were violent.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Likewise, he will open their ears to his correction, and he will speak to them, so that they may return from iniquity.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
If they listen and obey, they will fill their days with goodness and complete their years in glory.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
But if they will not listen, they will pass away by the sword and will be consumed by foolishness.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
The false and the crafty provoke the wrath of God, yet they do not cry out to him when they are chained.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Their soul will die in a storm, and their life, among the unmanly.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
He will rescue the poor from his anguish, and he will open his ear during tribulation.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Therefore, he will save you from the narrow mouth very widely, even though it has no foundation under it. Moreover, your respite at table will be full of fatness.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Your case has been judged like that of the impious; you will withdraw your plea and your judgment.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Therefore, do not let anger overwhelm you so that you oppress another; neither should you allow a multitude of gifts to influence you.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Lay down your greatness without distress, and put aside all of your power with courage.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Do not prolong the night, even if people rise on their behalf.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Be careful that you do not turn to iniquity; for, after your misery, you have begun to follow this.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Behold, God is exalted in his strength, and there is no one like him among the law-givers.
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Who is able to investigate his ways? And who can say, “You have done iniquity,” to him?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Remember that you are ignorant of his work, yet men have sung its praises.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
All men consider him; and each one ponders from a distance.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Behold, God is great, defeating our knowledge; the number of his years is inestimable.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
He carries away the drops of rain, and he sends forth showers like a raging whirlpool;
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
they flow from the clouds that are woven above everything.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
If he wills it, he extends the clouds as his tent
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
and shines with his light from above; likewise, he covers the oceans within his tent.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
For he judges the people by these things, and he gives food to a multitude of mortals.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Within his hands, he hides the light, and he commands it to come forth again.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
He announces it to his friend, for it is his possession and he is able to reach out to it.

< Ayubu 36 >