< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Elihu nastavi i reče:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
“Strpi se malo, pa ću te poučit', jer još nisam sve rekao za Boga.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Izdaleka ću svoje iznijet' znanje da Stvoritelja svojega opravdam.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Zaista, za laž ne znaju mi riječi, uza te je čovjek znanjem savršen.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Gle, Bog je silan, ali ne prezire, silan je snagom razuma svojega.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
Opakome on živjeti ne daje, nevoljnicima pravicu pribavlja.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
S pravednika on očiju ne skida, na prijestolje ih diže uz kraljeve da bi dovijeka bili uzvišeni.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
Ako su negvam' oni okovani i užetima nevolje sputani,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
djela njihova on im napominje, kazuje im grijeh njine oholosti.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Tad im otvara uho k opomeni i poziva ih da se zla okane.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
Poslušaju li te mu se pokore, dani im završavaju u sreći, u užicima godine njihove.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Ne slušaju li, od koplja umiru, zaglave, sami ne znajući kako.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
A srca opaka mržnju njeguju, ne ištu pomoć kad ih on okuje;
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
u cvatu svoga dječaštva umiru i venu poput hramskih milosnika.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Nevoljnog on bijedom njegovom spasava i u nesreći otvara mu oči:
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
izbavit će te iz ždrijela tjeskobe k prostranstvima bezgraničnim izvesti, k prepunu stolu mesa pretiloga.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Ako sudio nisi opakima, ako si pravo krnjio siroti,
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
nek' te obilje odsad ne zavede i nek' te dar prebogat ne iskvari.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Nek' ti je gavan k'o čovjek bez zlata, a čovjek jake ruke poput slaba.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Ne goni one koji su ti tuđi da rodbinu na njino mjesto staviš.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Pazi se da u nepravdu ne skreneš, jer zbog nje snađe tebe iskušenje.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Gle, uzvišen je Bog u svojoj snazi! Zar učitelja ima poput njega?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Tko je njemu put njegov odredio? Tko će mu reći: 'Radio si krivo'?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Spomeni se veličati mu djelo što ga pjesmama ljudi opjevaše.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
S udivljenjem svijet čitav ga promatra, divi se čovjek, pa ma izdaleka.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Veći je Bog no što pojmit' možemo, nedokučiv je broj ljeta njegovih!
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
U visini on skuplja kapi vode te dažd u paru i maglu pretvara.
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
Pljuskovi tada pljušte iz oblaka, po mnoštvu ljudskom dažde obilato.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
Tko li će shvatit' širenje oblaka, tutnjavu strašnu njegovih šatora?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Gle, on nad sobom razastire svjetlost i dno morsko on vodama pokriva.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Pomoću njih on podiže narode, u izobilju hranom ih dariva.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
On munju drži objema rukama i kazuje joj kamo će zgoditi.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
Glasom gromovnim sebe navješćuje, stiže s gnjevom da zgromi opačinu.

< Ayubu 36 >