< Ayubu 36 >
1 Elihu akaendelea kusema:
厄里烏又接著說:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
你且等一會,容我教導你,因為為天主,我還有些話要說。
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
我要將我所知的傳到遠方,將正義歸於我的造主。
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
的確,我的話正確無偽,知識全備的人同你一起。
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
的確,天主寬宏大量,決不藐視任何人,並且有廣大的同情心。
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
他決不容許惡人生存,但給窮苦人伸冤;
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
他也不剝奪義人的權利。他使君王永久坐在寶座上,但是他們卻驕矜自大;
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
故此,當他們一旦被鎖鏈束縛,被痛苦的繩索所繫,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
天主就向他們指明他們的惡行,和他們所誇耀的過犯,
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
開啟他們的耳朵,以聽訓戒,囑咐他們離開邪惡。
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
如果他們服從順命,便能幸福地度過歲月,能安樂地享受天年。
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
如果不服從,必被射死,於不知不覺中逝去。
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
心術敗壞的人,憤怒填胸,縱被囚禁,仍不呼求救助;
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
他們必早年夭折,喪命如男倡。
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
所以天主藉痛苦拯救受難的人,以患難開啟他們的耳鼓。
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
他也要救你擺脫災難,領你到廣闊自由之地,在你桌上常擺滿肥饌美味;
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
無如你判斷與惡人完全一樣,那麼懲罰和判案必集於你身。
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
小心! 不要讓忿怒引你肆口謾罵,也不要為重罰讓你離棄正道。
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
你的哀號和你所有的力量,豈能使你擺脫患難﹖
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
不要希望黑夜,那是人民由本地被劫去的時候。
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
小心! 別傾向不義,因為這正是你遭難的真正原因。
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
天主的能力確實偉大,那有像他那樣的主宰﹖
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
誰能規定他的道路,誰敢說:你行的不對﹖
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
你應記住要讚頌他的工程,這是人們應歌詠的。
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
人人都能觀賞,都能從遠處仰望:
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
天主何其偉大,我們不能理解! 他的歲數,無法考究。
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
他汲取水滴,使水氣化為雨露,
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
雨即從雲中傾盆而降,沛然落在眾人身上。
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
但誰能明瞭雲彩怎樣散布,天幕中怎樣發出隆隆之聲﹖
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
他將雲霧展開,遮蓋了群山山頂。
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
他藉此養育萬民,賜給他們豐富的食糧。
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
他掌中握著電光,對準目標發射出去。
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
雷霆報告他的來臨,他的怒火將要懲罰邪惡。