< Ayubu 34 >
ADEMÁS respondió Eliú, y dijo:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
Oid, sabios, mis palabras; y vosotros, doctos, estadme atentos.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
Porque el oído prueba las palabras, como el paladar gusta para comer.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Escojamos para nosotros el juicio, conozcamos entre nosotros cuál [sea] lo bueno:
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
Porque Job ha dicho: Yo soy justo, y Dios me ha quitado mi derecho.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
¿He de mentir yo contra mi razón? Mi saeta es gravosa sin [haber yo] prevaricado.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
¿Qué hombre hay como Job, que bebe el escarnio como agua?
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
Y va en compañía con los que obran iniquidad, y anda con los hombres maliciosos.
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
Porque ha dicho: De nada servirá al hombre el conformar su voluntad con Dios.
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
Por tanto, varones de seso, oidme: Lejos esté de Dios la impiedad, y del Omnipotente la iniquidad.
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
Porque él pagará al hombre según su obra, y él le hará hallar conforme á su camino.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Sí, por cierto, Dios no hará injusticia, y el Omnipotente no pervertirá el derecho.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
¿Quién visitó por él la tierra? ¿y quién puso en orden todo el mundo?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
Si él pusiese sobre el [hombre] su corazón, y recogiese así su espíritu y su aliento,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
Toda carne perecería juntamente, y el hombre se tornaría en polvo.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
Si pues [hay en ti] entendimiento, oye esto: escucha la voz de mis palabras.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
¿Enseñorearáse el que aborrece juicio? ¿y condenarás tú al que es tan justo?
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
¿Hase de decir al rey: Perverso; y á los príncipes: Impíos?
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
¿[Cuánto menos á] aquel que no hace acepción de personas de príncipes, ni el rico es de él más respetado que el pobre? porque todos son obras de sus manos.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
En un momento morirán, y á media noche se alborotarán los pueblos, y pasarán, y sin mano será quitado el poderoso.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
Porque sus ojos están sobre los caminos del hombre, y ve todos sus pasos.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
No hay tinieblas ni sombra de muerte donde se encubran los que obran maldad.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
No carga pues él al hombre más [de lo justo], para que vaya con Dios á juicio.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
El quebrantará á los fuertes sin pesquisa, y hará estar otros en su lugar.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
Por tanto él hará notorias las obras de ellos, cuando los trastornará en la noche, y serán quebrantados.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Como á malos los herirá en lugar donde sean vistos:
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
Por cuanto así se apartaron de él, y no consideraron todos sus caminos;
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
Haciendo venir delante de él el clamor del pobre, y que oiga el clamor de los necesitados.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
Y si él diere reposo, ¿quién inquietará? si escondiere el rostro, ¿quién lo mirará? [Esto] sobre una nación, y lo mismo sobre un hombre;
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
Haciendo que no reine el hombre hipócrita para vejaciones del pueblo.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
De seguro conviene se diga á Dios: Llevado he ya [castigo], no [más] ofenderé:
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
Enséñame tú lo que yo no veo: que si hice mal, no lo haré más.
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
¿[Ha de ser eso] según tu mente? El te retribuirá, ora rehuses, ora aceptes, y no yo: di si no, lo que tú sabes.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Los hombres de seso dirán conmigo, y el hombre sabio me oirá:
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
Que Job no habla con sabiduría, y que sus palabras no son con entendimiento.
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
Deseo yo que Job sea probado ampliamente, á causa de sus respuestas por los hombres inicuos.
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
Porque á su pecado añadió impiedad: bate las manos entre nosotros, y contra Dios multiplica sus palabras.