< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
Eliú continuó:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
Escuchen, oh sabios, mis palabras, y ustedes, los que saben, escúchenme.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
Porque el oído distingue las palabras y el paladar prueba el alimento.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Escojamos lo que es recto y sepamos entre nosotros lo que es bueno.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
Porque Job dijo: Yo soy justo. ʼEL me quitó mi derecho.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
¿Debo mentir con respecto a mi derecho? Aunque no cometí transgresión, mi herida es incurable.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
¿Quién hay como Job, quien bebe el desprecio como agua,
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
quien se va en compañía con los transgresores y camina con los perversos?
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
Pues afirma: De nada le sirve al hombre deleitarse en ʼElohim.
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
Por tanto, hombres cuerdos, escúchenme: ¡Lejos esté de ʼElohim la perversidad, y de ʼEL-Shadday la injusticia!
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
Porque Él paga al hombre según sus obras y hace que cada uno halle según su camino.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Ciertamente ʼElohim no obra perversamente, ni ʼEL-Shadday pervierte la justicia.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
¿Quién le dio autoridad sobre la tierra? ¿Quién le confió todo el universo?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
Si Él determina hacer así, retirar para Sí mismo su Espíritu y su aliento,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
toda carne perecería juntamente, y el hombre volvería al polvo.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
Si tienes entendimiento, escucha esto, escucha el sonido de mis palabras:
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
¿Gobernará el que aborrece la justicia? ¿Te atreves a condenar al Justo poderoso,
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
a Aquél que declara a un rey inútil y perversos a los nobles,
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
Quien no muestra parcialidad con príncipes, ni considera al rico por encima del pobre? Porque todos ellos son la obra de sus manos.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
De repente a medianoche mueren, las gentes se estremecen y ya no están. Los poderosos son derribados y no por mano.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
Porque los ojos de Él están sobre las sendas del hombre y observan todos sus pasos.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
No hay oscuridad ni sombras donde puedan ocultarse los que hacen iniquidad.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
Pues no le impone plazo al hombre, para que comparezca a juicio ante ʼEL.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
Él quebranta a los poderosos sin indagar y pone a otros en lugar de ellos.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
Por cuanto conoce las obras de ellos, los trastorna en una noche, y quedan deshechos.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Los azota por sus perversidades en un lugar público,
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
porque se apartaron de seguirlo. No consideraron alguno de los caminos de Él.
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
Buscaron que el clamor del pobre llegara a Él, y que escuchara el clamor de los afligidos.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
Cuando Él da tranquilidad, ¿quién entonces lo inculpará? Si esconde su rostro, ¿quién lo mirará? Esto ocurre tanto con respecto a una nación como con respecto a un hombre,
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
para evitar que reine el impío e imponga trampas al pueblo.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
Porque, ¿alguno le dijo a ʼEL: Generé mi castigo, no pecaré más,
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
enséñame Tú lo que yo no veo? ¡Si obré mal, no lo haré más!
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
¿Retribuirá según tus condiciones, porque tú rechazas las de Él? Si rechazas o si aceptas, Él te retribuirá, no yo. Y si no es así, dí lo que sabes.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Los hombres de entendimiento me lo dirán, y el hombre sabio que me escucha:
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
Que Job no habló con sabiduría, que sus palabras fueron sin discernimiento,
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
que Job debe ser probado hasta el límite, porque respondió como los perversos,
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
y a su pecado añade rebelión. Bate palmas ante nosotros y multiplica sus palabras contra ʼEL.

< Ayubu 34 >