< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
엘리후가 말을 이어 가로되
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
지혜 있는 자들아 내 말을 들으며 지식 있는 자들아 내게 귀를 기울이라
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
입이 식물의 맛을 변별함 같이 귀가 말을 분별하나니
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
우리가 스스로 옳은 것은 택하고 무엇이 선한가 우리끼리 알아보자
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
욥이 말하기를 내가 의로우나 하나님이 내 의를 제하셨고
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
내가 정직하나 거짓말장이가 되었고 나는 허물이 없으나 내 상처가 낫지 못하게 되었노라 하니
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
어느 사람이 욥과 같으랴 욥이 훼방하기를 물마시듯 하며
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
악한 일을 하는 자들과 사귀며 악인과 함께 다니면서
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
이르기를 사람이 하나님을 기뻐하나 무익하다 하는구나
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
그러므로 너희 총명한 자들아 내 말을 들으라 하나님은 단정코 악을 행치 아니하시며 전능자는 단정코 불의를 행치 아니하시고
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
사람의 일을 따라 보응하사 각각 그 행위대로 얻게 하시나니
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
진실로 하나님은 악을 행치 아니하시며 전능자는 공의를 굽히지 아니하시느니라
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
누가 땅을 그에게 맡겼느냐 누가 온 세계를 정하였느냐
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
그가 만일 자기만 생각하시고 그 신과 기운을 거두실진대
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
모든 혈기 있는 자가 일체로 망하고 사람도 진토로 돌아가리라
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
만일 총명이 있거든 이것을 들으며 내 말소리에 귀를 기울이라
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
공의를 미워하는 자시면 어찌 치리하시겠느냐 의롭고 전능하신 자를 네가 정죄하겠느냐
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
그는 왕에게라도 비루하다 하시며 귀인들에게라도 악하다 하시며
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
왕족을 외모로 취치 아니하시며 부자를 가난한 자보다 더 생각하지 아니하시나니 이는 그들이 다 그의 손으로 지으신 바가 됨이니라
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
그들은 밤중 순식간에 죽나니 백성은 떨며 없어지고 세력있는 자도 사람의 손을 대지 않고 제함을 당하느니라
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
하나님은 사람의 길을 주목하시며 사람의 모든 걸음을 감찰하시나니
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
악을 행한 자는 숨을 만한 흑암이나 어두운 그늘이 없느니라
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
하나님은 사람을 심판하시기에 오래 생각하실 것이 없으시니
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
세력 있는 자를 조사할 것 없이 꺾으시고 다른 사람을 세워 그를 대신하게 하시느니라
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
이와 같이 그들의 행위를 아시고 그들을 밤 사이에 엎으신즉 멸망하나니
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
그들을 악한 자로 여겨 사람의 목전에서 치심은
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
그들이 그를 떠나고 그의 모든 길을 무관히 여김이라
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
그들이 이와 같이 하여 가난한 자의 부르짖음이 그에게 상달케 하며 환난 받는 자의 부르짖음이 그에게 들리게 하느니라
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
주께서 사람에게 평강을 주실 때에 누가 감히 잘못하신다 하겠느냐 주께서 자기 얼굴을 가리우실 때에 누가 감히 뵈올 수 있으랴 나라에게나 사람에게나 일반이시니
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
이는 사특한 자로 권세를 잡아 백성을 함해하지 못하게 하려 하심이니라
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
누가 하나님께 아뢰기를 내가 징계를 받았사오니 다시는 범죄치 아니하겠나이다
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
나의 깨닫지 못하는 것을 내게 가르치소서 내가 악을 행하였으면 다시는 아니하겠나이다 한 자가 있느냐
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
하나님이 네 뜻대로 갚으셔야 하겠다고 네가 그것을 싫어하느냐 그러면 네가 스스로 택할 것이요 내가 할 것이 아니니 너는 아는대로 말하라
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
총명한 자와 내 말을 듣는 모든 지혜 있는 자가 필연 내게 이르기를
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
욥이 무식하게 말하니 그 말이 지혜 없다 하리라
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
욥이 끝까지 시험받기를 내가 원하노니 이는 그 대답이 악인과 같음이라
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
그가 그 죄 위에 패역을 더하며 우리 중에서 손뼉을 치며 하나님을 거역하는 말을 많이 하는구나

< Ayubu 34 >