< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
And Elihu commenced, and said,
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
Hear, O ye wise men, my words; and ye that have knowledge, give ear unto me.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
For the ear proveth words, as the palate tasteth the food.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Let us choose for ourselves what is just: let us acknowledge between ourselves what is good.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
For Job hath said, “I am righteous; and God hath taken away justice from me.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
Should I lie concerning the justice due me? incurable is [my wound from] the arrow I bear in me without any transgression.”
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
What man is there like Job, who drinketh scorning like water,
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
And is on the road to keep company with the wrong-doers, and to walk with men of wickedness?
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
For he hath said, “It profiteth a man nothing when he acteth according to the pleasure of God.”
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
Therefore ye men of sense hearken unto me: far is it from God to practise wickedness; and from the Almighty to do wrong!
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
For the work of a son of earth doth he recompense unto him, and according to the path of man doth he permit things to occur to him.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Yea, surely God will not condemn unjustly, nor will the Almighty pervert justice.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
Who hath given him a charge concerning the earth? or who hath intrusted [him] the whole world?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
If he were to set his heart upon man, he would gather unto himself his spirit and his breath:
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
All flesh would perish together, and the son of earth would return again unto dust.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
If then thou wishest to understand, hear this: give ear to the sound of my words.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
Is it possible that he who hateth justice should govern? or wilt thou condemn the righteous mighty One?
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
[Is it fit] to say to a king, Thou art worthless? and to princes, Ye are wicked?
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
Whereas he is one that showeth no favor to chieftains, and distinguisheth not the rich before the indigent; for all of them are the work of his hands.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
In a moment will they die, and in the midst of the night; people are moved, and pass away: and the mighty will be removed without a human hand.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
For big eyes are upon the ways of man, and all his steps doth he see.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
There is no darkness, nor shadow of death, where the evil-doers can hide themselves.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
For he need not direct [his attention] a long time upon man, that he should enter into judgment before God.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
He breaketh down mighty men without [long] searching, and placeth others in their stead.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
For the reason that he knoweth their deeds: therefore he overturneth them in the night, and they are crushed.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Among wicked men doth he strike them, in the place where [many] see them:
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
Because they have departed from following him, and have not considered all his ways.
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
Bringing before them the cry of the indigent, and the cry of the afflicted which he had to hear.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
When he now granteth rest, who will condemn [him]! and when he hideth his face, who can behold him? whether it be against a nation, or against one man, it is the same:
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
That no hypocritical man may reign, that such shall not be a mare to the people.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
For truly it is only fitting to say unto God, “I bear [cheerfully], I will not do any wrong;
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
What I cannot see myself, do thou truly teach me; if I have done what is unjust, I will do so no more.”
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
Should he then according to thy view send a recompense, because thou hast rejected him? “Because thou must choose, and not I?” and what thou knowest, do speak.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Men of sense will say unto me, and every wise man who heareth me,
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
That Job hath not spoken with knowledge, and that his words are without intelligence.
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
Oh that Job may therefore be probed continually, in order to give answers against sinful men.
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
For he addeth unto his sin transgression: among us he uttereth too many loud words, and multiplieth his speeches against God.

< Ayubu 34 >