< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
And Elius continued, and said,
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
Hear me, you wise men; listen, you that have knowledge.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
For the ear tries words, and the mouth tastes meat.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Let us choose judgment to ourselves: let us know amount ourselves what is right.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
For Job has said, I am righteous: the Lord has removed my judgment.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
And he has erred in my judgment: my wound is severe without unrighteousness [of mine].
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
What man is as Job, drinking scorning like water?
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
[saying], I have not sinned, nor committed ungodliness, nor had fellowship with workers of iniquity, to go with the ungodly.
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
For you should not say, There shall be no visitation of a man, whereas [there is] a visitation on him from the Lord.
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
Therefore hear me, you that are wise in heart: far be it from me to sin before the Lord, and to pervert righteousness before the almighty.
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
Yes, he renders to a man accordingly as each of them does, and in a man's path he will find him.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
And think you that the Lord will do wrong, or will the Almighty who made the earth wrest judgment?
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
And who is he that made [the whole world] under heaven, and all things therein?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
For if he would confine, and restrain his spirit with himself;
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
all flesh would die together, and every mortal would return to the earth, whence also he was formed.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
Take heed lest he rebuke [you]: hear this, listen to the voice of words.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
Behold then the one that hates iniquities, and that destroys the wicked, who is for ever just.
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
[He is] ungodly that says to a king, You are a transgressor, [that says] to princes, O most ungodly one.
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
[Such a one] as would not reverence the face of an honorable man, neither knows how to give honor to the great, so as that their persons should be respected.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
But it shall turn out vanity to them, to cry and beseech a man; for they dealt unlawfully, the poor being turned aside [from their right].
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
For he surveys the works of men, and nothing of what they do has escaped him.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
Neither shall there be a place for the workers of iniquity to hide themselves.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
For he will not lay upon a man more [than right].
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
For the Lord looks down upon all men, who comprehends unsearchable things, glorious also and excellent things without number.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
Who discovers their works, and will bring night about [upon them], and they shall be brought low.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
And he quite destroys the ungodly, for they are seen before him.
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
Because they turned aside from the law of God, and did not regard his ordinances,
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
so as to bring before him the cry of the needy; for he will hear the cry of the poor.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
And he will give quiet, and who will condemn? and he will hide his face, and who shall see him? whether [it be done] against a nation, or against a man also:
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
causing a hypocrite to be king, because of the waywardness of the people.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
For [there is] one that says to the Mighty One, I have received [blessings]; I will not take a pledge:
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
I will see apart from myself: do you show me if I have done unrighteousness; I will not do [so] any more.
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
Will he take vengeance for it on you, whereas you will put [it] far [from you]? for you shall choose, and not I; and what you know, speak you.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Because the wise in heart shall say this, and a wise man listens to my word.
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
But Job has not spoken with understanding, his words are not [uttered] with knowledge.
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
Howbeit do you learn, Job: no longer make answer as the foolish:
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
that we add not to our sins: for iniquity will be reckoned against us, if [we] speak many words before the Lord.

< Ayubu 34 >