< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
After proclaiming these things, Eliu now had this to say:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
May the wise hear my words, and may the educated listen to me.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
For the ear examines words, and the mouth discerns foods by the taste.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Let us choose judgment for ourselves, and let us consider among ourselves what is best.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
For Job has said: “I am just, yet God has subverted my judgment.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
For, within my judgment, there is a lie: my vehement barbs are without any sin.”
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
What man is there that is like Job, who drinks up derision as if it were water,
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
who accompanies those who work iniquity, and who walks with impious men?
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
For he has said, “Man will not please God, even if he should travel with him.”
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
Therefore, prudent men, hear me: impiety is far from God, and iniquity is far from the Almighty.
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
For he will restore to man his works, and according to the ways of each, he will repay them.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
For truly, God will not condemn in vain, nor will the Almighty repudiate judgment.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
What other is established over the earth? Or whom has he placed over the world, which he made?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
But, if he directs his heart towards him, he will draw his spirit and breath to himself.
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
All flesh will fail together, and man will return to ashes.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
Therefore, if you have understanding, hear what is said, and heed the sound of my eloquence.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
Is he that does not love judgment able to be corrected? And how can you so greatly condemn him who is just?
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
He says to the king, “You are an apostate.” He calls commanders impious.
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
He does not accept the reputation of leaders; nor does he recognize the tyrant as he contends against the poor. For all are the work of his hands.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
They will die suddenly, and the people will be troubled in the middle of the night, but they will pass through it, and the violent will be taken away without a hand.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
For his eyes are upon the ways of men, and he examines all of their steps.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
There is no darkness and no shadow of death, where those who work iniquity may be hidden.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
For it is no longer within the power of man to enter into judgment with God.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
He will break into many innumerable pieces, and he will cause others to stand up in their place.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
For he knows their works, and, as a result, he will bring the night, and they will be crushed.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Just as the impious do, he has struck them in a place where they can be seen.
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
They, as if with great diligence, have withdrawn from him, and they refused to understand all his ways,
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
so that they caused the outcry of the needy to reach him, and he heard the voice of the poor.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
For, when he grants peace, who is there that can condemn? When he hides his face, who is there that can contemplate him, either among the nations, or among all men?
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
He causes a hypocritical man to reign because of the sins of the people.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
Therefore, since I have been speaking about God, I will not prevent you from doing the same.
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
If I have erred, you may teach me; if I have spoken unfairly, I will add no more.
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
Does God require this of you because it is displeasing to you? For you were the first to speak, and not I. But if you know something better, speak.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Let men of understanding speak to me, and let a wise man listen to me.
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
But Job has been speaking foolishly, and his words contain unsound teaching.
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
My father, let Job be tested even to the end; may you not retreat from a man of iniquity.
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
For he adds blasphemy on top of his sins; nevertheless, let him be constrained to be among us, and then let him provoke God to judgment with his speeches.

< Ayubu 34 >