< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
Then Elihu continued:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
“Hear my words, O wise men; give ear to me, O men of learning.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
For the ear tests words as the mouth tastes food.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Let us choose for ourselves what is right; let us learn together what is good.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
For Job has declared, ‘I am righteous, yet God has deprived me of justice.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
Would I lie about my case? My wound is incurable, though I am without transgression.’
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
What man is like Job, who drinks up derision like water?
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
He keeps company with evildoers and walks with wicked men.
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
For he has said, ‘It profits a man nothing that he should delight in God.’
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
Therefore listen to me, O men of understanding. Far be it from God to do wrong, and from the Almighty to act unjustly.
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
For according to a man’s deeds He repays him; according to a man’s ways He brings consequences.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Indeed, it is true that God does not act wickedly, and the Almighty does not pervert justice.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
Who gave Him charge over the earth? Who appointed Him over the whole world?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
If He were to set His heart to it and withdraw His Spirit and breath,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
all flesh would perish together and mankind would return to the dust.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
If you have understanding, hear this; listen to my words.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
Could one who hates justice govern? Will you condemn the just and mighty One,
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
who says to kings, ‘You are worthless!’ and to nobles, ‘You are wicked,’
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
who is not partial to princes and does not favor rich over poor? For they are all the work of His hands.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
They die in an instant, in the middle of the night. The people convulse and pass away; the mighty are removed without human hand.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
For His eyes are on the ways of a man, and He sees his every step.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
There is no darkness or deep shadow where the workers of iniquity can hide.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
For God need not examine a man further or have him approach for judgment.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
He shatters the mighty without inquiry and sets up others in their place.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
Therefore, He recognizes their deeds; He overthrows them in the night and they are crushed.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
He strikes them for their wickedness in full view,
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
because they turned aside from Him and had no regard for any of His ways.
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
They caused the cry of the poor to come before Him, and He heard the outcry of the afflicted.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
But when He remains silent, who can condemn Him? When He hides His face, who can see Him? Yet He watches over both man and nation,
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
that godless men should not rule or lay snares for the people.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
Suppose someone says to God, ‘I have endured my punishment; I will offend no more.
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
Teach me what I cannot see; if I have done wrong, I will not do it again.’
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
Should God repay you on your own terms when you have disavowed His? You must choose, not I; so tell me what you know.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Men of understanding will declare to me, and the wise men who hear me will say:
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
‘Job speaks without knowledge; his words lack insight.’
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
If only Job were tried to the utmost for answering like a wicked man.
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
For he adds rebellion to his sin; he claps his hands among us and multiplies his words against God.”

< Ayubu 34 >