< Ayubu 34 >
Elihu nastavi svoju besjedu i reče:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
“I vi, mudraci, čujte što ću reći, vi, ljudi umni, poslušajte mene,
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
jer uši nam prosuđuju besjede isto kao što nepce hranu kuša.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Zajedno ispitajmo što je pravo i razmislimo skupa što je dobro.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
Job je utvrdio: 'Ja sam pravedan, ali Bog meni pravdu uskraćuje.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
U pravu sam, a lašcem prave mene, nasmrt prostrijeljen, a bez krivnje svoje!'
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
Zar gdje čovjeka ima poput Joba koji porugu pije kao vodu,
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
sa zlikovcima koji skupa hodi i s opakima isti dijeli put?
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
On tvrdi: 'Kakva korist je čovjeku od tog što Bogu ugoditi želi?'
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
Stoga me čujte, vi ljudi pametni! Od Boga zlo je veoma daleko i nepravednost od Svemogućega,
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
te on čovjeku plaća po djelima, daje svakom po njegovu vladanju.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Odista, Bog zla nikada ne čini, niti Svesilni kad izvrće pravo.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
TÓa tko je njemu povjerio zemlju i vasioni svijet tko je stvorio?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
Kad bi on dah svoj u se povukao, kad bi čitav svoj duh k sebi vratio,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
sva bića bi odjednom izdahnula i u prah bi se pretvorio čovjek.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
Ako razuma imaš, slušaj ovo, prikloni uho glasu riječi mojih.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
Može li vladat' koji mrzi pravo? Najpravednijeg hoćeš li osudit'? -
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
Onog koji kaže kralju: 'Nitkove!' a odličniku govori: 'Zlikovče!'
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
Koji nije spram knezovima pristran i jednak mu je ubog i mogućnik, jer oni su djelo ruku njegovih?
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
Zaglave za tren, usred gluhe noći: komešaju se narodi, prolaze; ni od čije ruke moćni padaju.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
Jer, on nadzire pute čovjekove, pazi nad svakim njegovim korakom.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
Nema toga mraka niti crne tmine gdje bi se mogli zlikovci sakriti.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
Bog nikome unaprijed ne kaže kada će na sud pred njega stupiti.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
Bez saslušanja on satire jake i stavlja druge na njihovo mjesto.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
TÓa odveć dobro poznaje im djela! Sred noći on ih obara i gazi.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Ćuškom ih bije zbog zloće njihove na mjestu gdje ih svi vidjeti mogu.
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
Jer prestadoše za njime hoditi, zanemariše putove njegove
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
goneć uboge da vape do njega i potlačene da k njemu leleču.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
Al' miruje li, tko da njega gane? Zastre li lice, tko ga vidjet' može?
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
Nad pucima bdi k'o i nad čovjekom da ne zavlada tko narod zavodi.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
Kada bezbožnik Bogu svome kaže: 'Zavedoše me, više griješit neću.
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
Ne uviđam li, ti me sad pouči, i ako sam kad nepravdu činio, ubuduće ja činiti je neću!'
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
Misliš da Bog mora njega kazniti, dok ti zamisli njegove prezireš? Al' kada ti odlučuješ, a ne ja, mudrost nam svoju istresi dÓe sada!
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Svi ljudi umni sa mnom će se složit' i svatko razuman koji čuje mene:
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
Nepromišljeno Job je govorio, u riječima mu neima mudrosti.
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
Stoga, nek' se Job dokraja iskuša, jer odgovara poput zlikovaca;
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
a svom grijehu još pobunu domeće, među nama on plješće dlanovima i hule svoje na Boga gomila.”