< Ayubu 34 >

1 Kisha Elihu akasema:
以利戶又說:
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
你們智慧人要聽我的話; 有知識的人要留心聽我說。
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
因為耳朵試驗話語, 好像上膛嘗食物。
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
我們當選擇何為是, 彼此知道何為善。
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
約伯曾說:我是公義, 上帝奪去我的理;
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
我雖有理,還算為說謊言的; 我雖無過,受的傷還不能醫治。
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
誰像約伯, 喝譏誚如同喝水呢?
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
他與作孽的結伴, 和惡人同行。
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
他說:人以上帝為樂, 總是無益。
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
所以,你們明理的人要聽我的話。 上帝斷不致行惡; 全能者斷不致作孽。
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
他必按人所做的報應人, 使各人照所行的得報。
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
上帝必不作惡; 全能者也不偏離公平。
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
誰派他治理地, 安定全世界呢?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
他若專心為己, 將靈和氣收歸自己,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
凡有血氣的就必一同死亡; 世人必仍歸塵土。
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
你若明理,就當聽我的話, 留心聽我言語的聲音。
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
難道恨惡公平的可以掌權嗎? 那有公義的、有大能的,豈可定他有罪嗎?
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
他對君王說:你是鄙陋的; 對貴臣說:你是邪惡的。
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
他待王子不徇情面, 也不看重富足的過於貧窮的, 因為都是他手所造。
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
在轉眼之間,半夜之中, 他們就死亡。 百姓被震動而去世; 有權力的被奪去非借人手。
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
上帝注目觀看人的道路, 看明人的腳步。
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
沒有黑暗、陰翳能給作孽的藏身。
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
上帝審判人,不必使人到他面前再三鑒察。
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
他用難測之法打破有能力的人, 設立別人代替他們。
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
他原知道他們的行為, 使他們在夜間傾倒滅亡。
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
他在眾人眼前擊打他們, 如同擊打惡人一樣。
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
因為他們偏行不跟從他, 也不留心他的道,
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
甚至使貧窮人的哀聲達到他那裏; 他也聽了困苦人的哀聲。
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
他使人安靜,誰能擾亂呢? 他掩面,誰能見他呢? 無論待一國或一人都是如此-
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
使不虔敬的人不得作王, 免得有人牢籠百姓。
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
有誰對上帝說: 我受了責罰,不再犯罪;
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
我所看不明的,求你指教我; 我若作了孽,必不再作?
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
他施行報應, 豈要隨你的心願、叫你推辭不受嗎? 選定的是你,不是我。 你所知道的只管說吧!
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
明理的人和聽我話的智慧人必對我說:
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
約伯說話沒有知識, 言語中毫無智慧。
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
願約伯被試驗到底, 因他回答像惡人一樣。
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
他在罪上又加悖逆; 在我們中間拍手, 用許多言語輕慢上帝。

< Ayubu 34 >