< Ayubu 33 >
1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
“Ama şimdi lütfen sözümü dinle, Eyüp, Söyleyeceğim her şeye kulak ver.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Ağzımı açtım açacağım, Söyleyeceklerim dilimin ucunda.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Sözlerim temiz bir yürekten çıkıyor, Dudaklarım bildiklerini içtenlikle söylüyor.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
Beni Tanrı'nın Ruhu yarattı, Her Şeye Gücü Yeten'in soluğu yaşam veriyor bana.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Elinden gelirse beni yanıtla, Kendini hazırla, karşımda dur.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Tanrı'nın önünde ben de tıpkı senin gibiyim, Ben de balçıktan yaratıldım.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Onun için dehşetim seni yıldırmasın, Baskım sana ağır gelmesin.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
“Sesin hâlâ kulaklarımda, Şöyle demiştin:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
‘Ben kusursuz ve günahsızım, Temiz ve suçsuzum.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Yine de Tanrı bana karşı bahane arıyor, Beni düşman görüyor.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
Ayaklarımı tomruğa vuruyor, Yollarımı gözetliyor.’
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
“Ama sana şunu söyleyeyim, Bu konuda haksızsın. Çünkü Tanrı insandan büyüktür.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
İnsanın hiçbir sözünü yanıtlamıyor diye Niçin O'nunla çekişiyorsun?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
Çünkü insan anlamasa da, Tanrı şu ya da bu yolla konuşur.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
Rüyada, geceleyin görümde, İnsanları ağır uyku basınca, Yatakta yatarlarken,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Kulaklarına konuşur, Uyarısıyla onları korkutur;
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
Onları yaptıkları kötülükten döndürmek, Gururdan uzak tutmak,
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
Canlarını çukurdan, Hayatlarını ölümden kurtarmak için.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
İnsan yatağında acılarla, Kemiklerinde dinmez sızılarla yola getirilir.
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
Öyle ki, içi yemek kaldırmaz, En lezzetli yiyecekten tiksinir.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Eti erir, görünmez olur, Gözükmeyen kemikleri ortaya çıkar.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Canı çukura, Hayatı ölüm meleklerine yaklaşır.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
“Yine de insana doğruyu bildirmek için Yanında bir melek, bin melekten biri Arabulucu olarak bulunursa,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Ona lütfeder de, ‘Onu ölüm çukuruna inmekten kurtar, Ben fidyeyi buldum’ derse,
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Eti çocuk eti gibi yenilenir, Gençlik günlerine döner.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
Dua ettiğinde Tanrı ondan hoşnut kalır, O da Tanrı'nın yüzünü görüp sevinir. Tanrı onun durumunu düzeltir.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
Sonra insanların önünde türkü çağırır: ‘Günah işleyip doğru yoldan saptım, Ama Tanrı hak ettiğim cezayı vermedi bana,
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
Canımı çukura inmekten O kurtardı, Işığı görmek için yaşayacağım.’
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
“İşte, insanın canını çukurdan çıkarmak, Onu yaşam ışığıyla aydınlatmak için Tanrı bütün bunları iki kez, Hatta üç kez yapar.
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
“İyi dinle, Eyüp, kulak ver, Sen sus, ben konuşacağım.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Söyleyeceğin bir şey varsa söyle, Çünkü seni haklı çıkarmak isterim.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Yoksa, beni dinle, Sus da sana bilgelik öğreteyim.”