< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Sin embargo, Job, escucha ahora mis razones y atiende todas mis palabras.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Ciertamente ahora abro mi boca. Mi lengua habla en mi paladar.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Mis palabras declararán la rectitud de mi corazón y lo que saben mis labios lo dicen con sinceridad:
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
El Espíritu de ʼElohim me hizo y el soplo de ʼEL-Shadday me dio vida.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Respóndeme si puedes. Alístate y ponte en pie ante mí.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Ciertamente pertenezco a ʼEL, como tú. Del barro también fui formado.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Ciertamente mi terror no te espantará, ni mi mano será demasiado pesada sobre ti.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
En verdad tú dijiste a oídos míos. Yo oí el sonido de tus palabras:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
Limpio soy, sin transgresión. Soy inocente y no hay culpa en mí.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Ciertamente Él inventa pretextos contra mí y me considera su enemigo.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
Puso mis pies en el cepo y vigila todos mis pasos.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Ciertamente yo te respondo: En esto no eres justo, porque ʼElohim es mayor que el hombre.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
¿Por qué contiendes con ʼEL? Pues Él no da cuenta de ninguna de sus obras.
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
Porque ʼElohim habla de una manera o de otra, pero nadie lo percibe:
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
En sueño, en visión nocturna, cuando el sopor cae sobre los hombres, mientras se adormecen en la cama,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Él abre el oído de los hombres y sella su instrucción para ellos,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
a fin de apartar al hombre de su obra y destruir la soberbia del varón,
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
para librar su alma del sepulcro y que su vida no perezca a filo de espada.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
También sobre su cama es reprendido con dolores, con el dolor incesante de sus huesos,
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
lo cual hace que le repugne el pan, y aun el manjar más delicado.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Su carne se consume hasta que no se ve, y sus huesos, que no se veían, aparecen.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Su alma se acerca al sepulcro y su vida a los que causan la muerte.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
Si hay un ángel que sea mediador para él, muy escogido entre 1.000, que recuerda al hombre lo correcto para él,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
tenga compasión de él y diga: Líbrenlo de bajar al sepulcro, pues le hallé un rescate.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Entonces su carne sería más tierna que la de un joven que vuelve al vigor de los días de su juventud.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
Invocaría a ʼEloha. Él le haría sacrificio que apacigua, para que vea el semblante de ʼEL con gozo y Él le restaure su justicia al hombre.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
Él mira a los hombres y al que dice: Pequé y pervertí lo recto, pero nada me aprovechó,
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
Él le redimirá su alma para que no baje al sepulcro, y su vida verá la luz.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
En verdad ʼEL hace todas estas cosas con el hombre dos veces, y aun tres,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
para rescatar su alma del sepulcro e iluminarlo con la luz de la vida.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Presta atención, Job, escúchame. Calla, y permíteme hablar.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Si tienes palabras, respóndeme. Habla, porque yo quiero declararte justo.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Si no, escúchame. Calla, y yo te enseñaré sabiduría.

< Ayubu 33 >