< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
“Ahora escúchame, Job. Presta atención a todo lo que tengo que decir.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Mira, estoy a punto de hablar; mi boca está lista para hablar.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Mis palabras salen de mi corazón recto; mis labios hablan con sinceridad de lo que sé.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
El espíritu de Dios me hizo, y el aliento del Todopoderoso me da vida.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Contéstame, si puedes. Ponte delante de mí y prepárate para defenderte:
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Ante Dios los dos somos iguales. Yo también fui hecho de un pedazo de arcilla.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
No tienes que tener miedo de mí, pues no seré demasiado duro contigo.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Has hablado en mi oído y he escuchado todo lo que tenías que decir.
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
Dices: ‘Estoy limpio, no he hecho nada malo; soy puro, no he pecado.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Mira cómo Dios encuentra faltas en mí y me trata como su enemigo.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
Pone mis pies en el cepo y vigila todo lo que hago’.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Pero te equivocas. Déjame explicarte: Dios es más grande que cualquier ser humano.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
¿Por qué luchas contra él, quejándote de que Dios no responde a tus preguntas?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
Dios habla una y otra vez, pero la gente no se da cuenta.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
A través de sueños y visiones en la noche, cuando la gente cae en el sueño profundo, descansando en sus camas,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Dios les habla con advertencias solemnes
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
para alejarlos de hacer el mal y evitar que se vuelvan orgullosos.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
Los salva de la tumba y los libra de la muerte violenta.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
La gente también es disciplinada en un lecho de dolor, con un dolor constante en sus huesos.
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
No tienen deseos de comer; ni siquiera quieren sus platos favoritos.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Su carne se desgasta hasta quedar en nada; todo lo que queda es piel y huesos.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Están a punto de morir; su vida se acerca al verdugo.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
“Pero si aparece un ángel, un mediador, uno de los miles de ángeles de Dios, para indicarle a alguien el camino correcto para ellos,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
tendrá gracia con ellos. Les dirá: ‘Sálvenlos de bajar a la tumba, porque he encontrado un camino para liberarlos’.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Entonces sus cuerpos se renovarán como si fueran jóvenes de nuevo; serán tan fuertes como cuando estaban en la flor de la vida.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
Orarán a Dios, y él los aceptará; llegarán a la presencia de Dios con alegría, y él les arreglará las cosas.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
Cantarán y dirán a los demás: ‘He pecado, he desvirtuado lo que es justo, pero no me ha servido de nada.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
Me salvó de bajar al sepulcro y viviré en la luz’.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Mira, Dios hace esto una y otra vez para la gente;
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
los salva de la tumba para que vean la luz de la vida.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
“Presta atención, Job, y escúchame. Calla y déjame hablar.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Pero si tienes algo que decir, habla.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Si no, escúchame. Calla y te enseñaré la sabiduría”.

< Ayubu 33 >