< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Audi igitur Iob eloquia mea, et omnes sermones meos ausculta.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Ecce aperui os meum, loquatur lingua mea in faucibus meis.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Simplici corde meo sermones mei, et sententiam puram labia mea loquentur.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
Spiritus Dei fecit me, et spiraculum Omnipotentis vivificavit me.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Si potes, responde mihi, et adversus faciem meam consiste.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Ecce, et me sicut et te fecit Deus, et de eodem luto ego quoque formatus sum.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Verumtamen miraculum meum non te terreat, et eloquentia mea non sit tibi gravis.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Dixisti ergo in auribus meis, et vocem verborum tuorum audivi:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
Mundus sum ego, et absque delicto: immaculatus, et non est iniquitas in me.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Quia querelas in me reperit, ideo arbitratus est me inimicum sibi.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
Posuit in nervo pedes meos, custodivit omnes semitas meas.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Hoc est ergo, in quo non es iustificatus: respondebo tibi, quia maior sit Deus homine.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Adversus eum contendis quod non ad omnia verba responderit tibi?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
Semel loquitur Deus, et secundo idipsum non repetit.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
Per somnium in visione nocturna, quando irruit sopor super homines, et dormiunt in lectulo:
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Tunc aperit aures virorum, et erudiens eos instruit disciplina,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
Ut avertat hominem ab his, quæ facit, et liberet eum de superbia:
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
Eruens animam eius a corruptione: et vitam illius, ut non transeat in gladium.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
Increpat quoque per dolorem in lectulo, et omnia ossa eius marcescere facit.
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
Abominabilis ei fit in vita sua panis, et animæ illius cibus ante desiderabilis.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Tabescet caro eius, et ossa, quæ tecta fuerant, nudabuntur.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Appropinquavit corruptioni anima eius, et vita illius mortiferis.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
Si fuerit pro eo Angelus loquens, unus de millibus, ut annunciet hominis æquitatem:
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Miserebitur eius, et dicet: Libera eum, ut non descendat in corruptionem: inveni in quo ei propitier.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Consumpta est caro eius a suppliciis, revertatur ad dies adolescentiæ suæ.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
Deprecabitur Deum, et placabilis ei erit: et videbit faciem eius in iubilo, et reddet homini iustitiam suam.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
Respiciet homines, et dicet: Peccavi, et vere deliqui, et, ut eram dignus, non recepi.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
Liberavit animam suam ne pergeret in interitum, sed vivens lucem videret.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Ecce, hæc omnia operatur Deus tribus vicibus per singulos.
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
Ut revocet animas eorum a corruptione, et illuminet luce viventium.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Attende Iob, et audi me: et tace, dum loquor.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Si autem habes quod loquaris, responde mihi, loquere: volo enim, te apparere iustum.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Quod si non habes, audi me: tace, et docebo te sapientiam.

< Ayubu 33 >