< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
And yet, I pray thee, O Job, Hear my speech and [to] all my words give ear.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Lo, I pray thee, I have opened my mouth, My tongue hath spoken in the palate.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Of the uprightness of my heart [are] my sayings, And knowledge have my lips clearly spoken.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The Spirit of God hath made me, And the breath of the Mighty doth quicken me.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
If thou art able — answer me, Set in array before me — station thyself.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Lo, I [am], according to thy word, for God, From the clay I — I also, have been formed.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Lo, my terror doth not frighten thee, And my burden on thee is not heavy.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Surely — thou hast said in mine ears, And the sounds of words I hear:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
'Pure [am] I, without transgression, Innocent [am] I, and I have no iniquity.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Lo, occasions against me He doth find, He doth reckon me for an enemy to Him,
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He doth put in the stocks my feet, He doth watch all my paths.'
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Lo, [in] this thou hast not been righteous, I answer thee, that greater is God than man.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Wherefore against Him hast thou striven, When [for] all His matters He answereth not?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
For once doth God speak, and twice, (He doth not behold it.)
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
In a dream — a vision of night, In the falling of deep sleep on men, In slumberings on a bed.
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Then He uncovereth the ear of men, And for their instruction sealeth:
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
To turn aside man [from] doing, And pride from man He concealeth.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
He keepeth back his soul from corruption, And his life from passing away by a dart.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
And he hath been reproved With pain on his bed, And the strife of his bones [is] enduring.
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
And his life hath nauseated bread, And his soul desirable food.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
His flesh is consumed from being seen, And high are his bones, they were not seen!
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
And draw near to the pit doth his soul, And his life to those causing death.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
If there is by him a messenger, An interpreter — one of a thousand, To declare for man his uprightness:
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Then He doth favour him and saith, 'Ransom him from going down to the pit, I have found an atonement.'
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Fresher [is] his flesh than a child's, He returneth to the days of his youth.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
He maketh supplication unto God, And He accepteth him. And he seeth His face with shouting, And He returneth to man His righteousness.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He looketh on men, and saith, 'I sinned, And uprightness I have perverted, And it hath not been profitable to me.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He hath ransomed my soul From going over into the pit, And my life on the light looketh.'
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Lo, all these doth God work, Twice — thrice with man,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
To bring back his soul from the pit, To be enlightened with the light of the living.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Attend, O Job, hearken to me, Keep silent, and I — I do speak.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
If there are words — answer me, Speak, for I have a desire to justify thee.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
If there are not — hearken thou to me, Keep silent, and I teach thee wisdom.

< Ayubu 33 >