< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
“But now, Job, listen carefully to all that I am going to say [DOU].
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
I am ready to tell you [MTY, DOU] [what I think].
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
I know that I am speaking honestly and that I am speaking [MTY] sincerely.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
Almighty God has created me [as well as you], and his breath has caused me to live.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
So, answer [what] I [say] if you can; think carefully [about how you will reply to me].
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
“God considers that you, and I are both [equal]; he formed both of us from clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
So you do not need to be afraid of me; I will not crush/oppress you [by what I say] [MTY].
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
I have heard you [DOU] speaking, and this is what you have said:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
‘I am innocent; I have not committed any sins; I am pure; I have not done things that are wrong.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
But God finds reasons to accuse me, and he considers that I am his enemy.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
[It is as though] he has put my feet (in stocks/between wooden blocks to prevent me from walking away), and he watches everything that I do.’ [MTY]
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
But what you have said is wrong, and I will tell you [what you have said that is wrong]. God is much greater than any human.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
So, (why are you arguing against God, saying ‘He never answers my questions’?/you should not be arguing against God, saying ‘He never answers my questions.’) [RHQ]
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
God does speak [to us] in various ways, but we do not pay any attention to what he says.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
[Sometimes he speaks to us] at night in dreams and visions, when we are on our beds, asleep [DOU].
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
He reveals things [MTY] to us and terrifies us by the things he warns us about.
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
He tell us those things in order that we stop doing [evil] things and to prevent us from becoming proud.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
He does not want us to be destroyed [MTY]; he wants to prevent us from dying [MTY] [while we are still young].
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
God also [sometimes] corrects us by forcing us to lie on our beds suffering much pain and with fever/aching in our bones.
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
The result is that we do not desire any food, not even very special food.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Our bodies become very thin, with the result that we look like skeletons [HYP], and our bones stick out.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
[We know that] we will soon die and go to the place where dead people are.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
“But sometimes an angel [may come to one of us], one of the thousands of angels who come to intervene between us and God, to tell us what are the right things for us [to do].
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
The angel is kind to us and says to God, ‘Release that person, so that he does not descend to the place where dead people are! Do that because I have found the money to pay so that he can be released!
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Allow his body to be strong again; allow him to be strong like he was when he was a youth!’
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
When that happens, that person will pray to God, and God will accept/answer him; he will (enter God’s presence/worship God) joyfully, and then he will tell others how God saved him [from dying].
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He will sing as he tells everyone, ‘I sinned, and I did things that were not right, but God did not punish me in the way that I deserved.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He has saved me from dying and going to the place where dead people are, and I will continue to enjoy being alive.’
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
God does all these things for us many times;
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
he keeps us [SYN] from [dying and] going to the place where the dead are, in order that we can continue to enjoy being alive [IDM].
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
So Job, listen to me; do not say anything more; just allow me to speak.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
[After I speak], if you have something more that you want to say to me, say it, because I would like to find a way to declare that you (are innocent/have not done what is wrong).
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
But if you have nothing more that you want to say, then just listen to me, and I will teach you how to become wise.”

< Ayubu 33 >