< Ayubu 33 >
1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Hear, therefore, my discourse, I pray thee, O Job! And attend unto all my words!
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Behold, I am opening my mouth; My tongue is now speaking in my palate.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
My words shall be in the uprightness of my heart; My lips shall utter knowledge purely.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The spirit of God made me, And the breath of the Almighty gave me life.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
If thou art able, answer me; Set thyself in array against me; stand up!
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Behold, I, like thee, am a creature of God; I also was formed of clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Behold, my terror cannot dismay thee, Nor can my greatness be heavy upon thee.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Surely thou hast said in my hearing, I have heard the sound of thy words:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
“I am pure, and without transgression; I am clean, and there is no iniquity in me.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Behold, He seeketh causes of hostility against me; He regardeth me as his enemy.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He putteth my feet in the stocks; He watcheth all my paths.”
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Behold, in this thou art not right; I will answer thee; For God is greater than man.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Why dost thou contend with Him? For he giveth no account of any of his doings.
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
For God speaketh once, Yea, twice, when man regardeth it not.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
In a dream, in a vision of the night, When deep sleep falleth upon men, In slumber upon the bed;
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Then openeth he the ears of men, And sealeth up for them admonition;
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
That he may turn man from his purpose, And hide pride from man.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
Thus he saveth him from the pit, Yea, his life from perishing by the sword.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
He is chastened also with pain upon his bed, And with a continual agitation of his bones,
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
So that his mouth abhorreth bread, And his taste the choicest food;
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
His flesh is consumed, that it cannot be seen, And his bones, that were invisible, are naked;
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Yea, his soul draweth near to the pit, And his life to the destroyers.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
But if there be with him a messenger, An interpreter, one of a thousand, Who may show unto man his duty,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Then will God be gracious to him, and say, “Save him from going down to the pit: I have found a ransom.”
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
His flesh shall became fresher than a child's; He shall return to the days of his youth.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
He shall pray to God, and he will be favorable to him, And permit him to see his face with joy, And restore unto man his righteousness.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He shall sing among men, and say, “I sinned; I acted perversely; Yet hath he not requited me for it:
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He hath delivered me from going down to the pit, And my life beholdeth the light.”
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Lo! all these things doeth God Time after time with man,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
That he may bring him back from the pit, That he may enjoy the light of the living.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Mark well, O Job! hearken to me! Keep silence, and I will speak.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Yet if thou hast any thing to say, answer me! Speak! for I desire to pronounce thee innocent.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
But if not, do thou listen to me! Keep silence, and I will teach thee wisdom!