< Ayubu 33 >
1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Therefore do thou but hear, O Job, my speeches, and give ear to all my words.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Behold now, I have opened my mouth, my tongue speaketh in my mouth.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Out of my straightforward heart [come] my sayings, and my lips utter knowledge clearly.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The spirit of God hath made me, and the breath of the Almighty giveth me life.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
If thou canst, answer me, array thyself before me, stand forward.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Behold, I am in the same relation as thyself toward God: I myself also am cut out of the clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Behold, dread of me cannot terrify thee, and my pressure will not be too heavy upon thee.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
But thou hast said before my ears, and the sound of the words I still hear,
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
“I am pure without transgression, I am quite clean; and there is no iniquity in me:
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Yet, behold, he findeth hateful backsliding on me, he regardeth me as an enemy unto him;
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He putteth my feet in the stocks, he watcheth all my paths.”
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Behold, In this thou art not just: I will answer thee; for God is far greater than a mortal.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Why dost thou contend against him? for with all his words will he not give an answer.
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
For God speaketh once, yea twice: [yet man] regardeth it not.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falleth upon men, in slumbers upon the couch:
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Then doth he lay open the ear of men, and sealeth it with their warning;
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
To remove the son of earth [from his intended] deed and he covereth up pride from man;
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
He withholdeth his soul from the pit, and his life from passing away by the sword.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
And so is he admonished by pain upon his couch, and all his bones with violent [aches].
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
So that his inclination abhorreth bread, and his soul, the most agreeable food.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
His flesh is consumed away, that it cannot be seen, and his bones that were not seen stick out.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Yea, his soul draweth near unto the pit, and his life to those that slay.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
If there be now about him one single angel, as defender, one out of a thousand, to tell for man his uprightness:
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Then is he gracious unto him, and saith, Release him from going down to the pit, I have found an atonement.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
His flesh becometh full again as in youth: he returneth to the days of his boyhood.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
He will offer his entreaty unto God, and he will receive him in favor, that he may see his face with joy: so doth He recompense unto the mortal his righteousness.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He then should assemble men around, and say, “I had sinned, and perverted what is right, yet have I not received a like return.”
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
Thus he redeemeth his soul from passing into the pit, and his life will look joyously on the light.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Lo, all these things doth God two or three times with man;
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
To bring back his soul from the pit, that she may shine in the light of life.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Listen well, O Job, hearken unto me: keep silence, and I will truly speak.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
If thou hast any words, answer me: speak, for I wish to justify thee.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
If not, hearken thou unto me: keep silence, and I will teach thee wisdom.