< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Wherefore, Job, I pray you, hear my speeches, and hearken to all my words.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Behold, now I have opened my mouth, my tongue has spoken in my mouth.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
My words shall be of the uprightness of my heart: and my lips shall utter knowledge clearly.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The spirit of God has made me, and the breath of the Almighty has given me life.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
If you can answer me, set your words in order before me, stand up.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Behold, I am according to your wish in God's position: I also am formed out of the clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Behold, my terror shall not make you afraid, neither shall my hand be heavy upon you.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Surely you have spoken in mine hearing, and I have heard the voice of your words, saying,
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
I am clean without transgression, I am innocent; neither is there iniquity in me.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Behold, he finds occasions against me, he counts me for his enemy,
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He puts my feet in the stocks, he marks all my paths.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Behold, in this you are not just: I will answer you, that God is greater than man.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Why do you strive against him? for he gives not account of any of his matters.
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
For God speaks once, yea twice, yet man perceives it not.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falls upon men, in slumberings upon the bed;
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Then he opens the ears of men, and seals their instruction,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
That he may withdraw man from his purpose, and hide pride from man.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
He keeps back his soul from the pit, and his life from perishing by the sword.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
He is chastened also with pain upon his bed, and the multitude of his bones with strong pain:
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
So that his life detests bread, and his soul dainty food.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
His flesh is consumed away, that it cannot be seen; and his bones that were not seen stick out.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Yea, his soul draws near unto the grave, and his life to the destroyers.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
If there be a messenger with him, an interpreter, one among a thousand, to show unto man his uprightness:
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Then he is gracious unto him, and says, Deliver him from going down to the pit: I have found a ransom.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
His flesh shall be fresher than a child's: he shall return to the days of his youth:
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
He shall pray unto God, and he will be favourable unto him: and he shall see his face with joy: for he will render unto man his righteousness.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He looks upon men, and if any say, I have sinned, and perverted that which was right, and it profited me not;
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He will deliver his soul from going into the pit, and his life shall see the light.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Lo, all these things works God oftentimes with man,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
To bring back his soul from the pit, to be enlightened with the light of the living.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Mark well, O Job, hearken unto me: hold your peace, and I will speak.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
If you have anything to say, answer me: speak, for I desire to justify you.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
If not, hearken unto me: hold your peace, and I shall teach you wisdom.

< Ayubu 33 >