< Ayubu 33 >
1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Wherefore, Iob, I pray thee, heare my talke and hearken vnto all my wordes.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Beholde now, I haue opened my mouth: my tongue hath spoken in my mouth.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
My words are in the vprightnesse of mine heart, and my lippes shall speake pure knowledge.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The Spirite of God hath made me, and the breath of the Almightie hath giuen me life.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
If thou canst giue me answere, prepare thy selfe and stand before me.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Beholde, I am according to thy wish in Gods stead: I am also formed of the clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Beholde, my terrour shall not feare thee, neither shall mine hand be heauie vpon thee.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Doubtles thou hast spoken in mine eares, and I haue heard the voyce of thy wordes.
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
I am cleane, without sinne: I am innocent, and there is none iniquitie in me.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Lo, he hath found occasions against me, and counted me for his enemie.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He hath put my feete in the stockes, and looketh narrowly vnto all my paths.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Behold, in this hast thou not done right: I will answere thee, that God is greater then man.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Why doest thou striue against him? for he doeth not giue account of all his matters.
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
For God speaketh once or twise, and one seeth it not.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
In dreames and visions of the night, when sleepe falleth vpon men, and they sleepe vpon their beds,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Then he openeth the eares of men, euen by their corrections, which he had sealed,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
That he might cause man to turne away from his enterprise, and that he might hide the pride of man,
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
And keepe backe his soule from the pit, and that his life should not passe by the sword.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
He is also striken with sorow vpon his bed, and the griefe of his bones is sore,
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
So that his life causeth him to abhorre bread, and his soule daintie meate.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
His flesh faileth that it can not be seene, and his bones which were not seene, clatter.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
So his soule draweth to the graue, and his life to the buriers.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
If there be a messenger with him, or an interpreter, one of a thousand to declare vnto man his righteousnesse,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Then will he haue mercie vpon him, and will say, Deliuer him, that he go not downe into the pit: for I haue receiued a reconciliation.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Then shall his flesh be as fresh as a childes, and shall returne as in the dayes of his youth.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
He shall pray vnto God, and he will be fauourable vnto him, and he shall see his face with ioy: for he will render vnto man his righteousnes.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He looketh vpon men, and if one say, I haue sinned, and peruerted righteousnesse, and it did not profite me,
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He will deliuer his soule from going into the pit, and his life shall see the light.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Lo, all these things will God worke twise or thrise with a man,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
That he may turne backe his soule from the pit, to be illuminate in the light of the liuing.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Marke well, O Iob, and heare me: keepe silence, and I will speake.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
If there be matter, answere me, and speak: for I desire to iustifie thee.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
If thou hast not, heare me: holde thy tongue, and I will teach thee wisedome.