< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Howbeit, Job, I pray thee, hear mine utterances, and hearken to all my words.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Behold now, I have opened my mouth, my tongue speaketh in my palate,
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
My words shall be of the uprightness of my heart, and my lips shall utter knowledge purely.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The Spirit of God hath made me, and the breath of the Almighty hath given me life.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
If thou canst, answer me; array [thy words] before me: take thy stand.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Behold, before God I am as thou; I also am formed out of the clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Behold, my terror shall not make thee afraid, nor my burden be heavy upon thee.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Surely thou hast spoken in my hearing, and I have heard the voice of [thy] words: —
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
I am clean without transgression; I am pure, and there is no iniquity in me;
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Lo, he findeth occasions of hostility against me, he counteth me for his enemy;
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He putteth my feet in the stocks, he marketh all my paths.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Behold, I will answer thee in this, thou art not right; for God is greater than man.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Why dost thou strive against him? for he giveth not account of any of his matters.
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
For God speaketh once, and twice, — [and man] perceiveth it not —
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falleth upon men, in slumberings upon the bed;
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Then he openeth men's ears, and sealeth their instruction,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
That he may withdraw man [from his] work, and hide pride from man.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
He keepeth back his soul from the pit, and his life from passing away by the sword.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
He is chastened also with pain upon his bed, and with constant strife in his bones;
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
And his life abhorreth bread, and his soul dainty food;
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
His flesh is consumed away from view, and his bones that were not seen stick out;
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
And his soul draweth near to the pit, and his life to the destroyers.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
If there be a messenger with him, an interpreter, one among a thousand, to shew unto man his duty;
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Then he will be gracious unto him, and say, Deliver him from going down to the pit: I have found a ransom.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
His flesh shall be fresher than in childhood; he shall return to the days of his youth.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
He shall pray unto God, and he will receive him with favour; and he shall see his face with shoutings, and he will render unto man his righteousness.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He will sing before men, and say, I have sinned, and perverted what was right, and it hath not been requited to me;
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He hath delivered my soul from going into the pit, and my life shall see the light.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Lo, all these [things] worketh God twice, thrice, with man,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
To bring back his soul from the pit, that he may be enlightened with the light of the living.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Mark well, Job, hearken unto me; be silent, and I will speak.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
If thou hast anything to say, answer me; speak, for I desire to justify thee.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
If not, hearken thou unto me; be silent, and I will teach thee wisdom.

< Ayubu 33 >