< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
However, Job, I pray thee, hear my speech, and hearken to all my words.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Behold now, I have opened my mouth. My tongue has spoken in my mouth.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
My words shall utter the uprightness of my heart, and that which my lips know they shall speak sincerely.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The Spirit of God has made me, and the breath of the Almighty gives me life.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
If thou can, answer thou me. Set thy words in order before me. Stand forth.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Behold, I am toward God even as thou are. I also am formed out of the clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Behold, my terror shall not make thee afraid, nor shall my pressure be heavy upon thee.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Surely thou have spoken in my hearing, and I have heard the voice of thy words, saying,
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
I am clean, without transgression. I am innocent, neither is there iniquity in me.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Thou say, Behold, he finds occasions against me. He counts me for his enemy.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He puts my feet in the stocks. He marks all my paths.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Behold, I will answer thee. In this thou are not just, for God is greater than man.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Why do thou strive against him because he does not give account of any of his matters?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
For God speaks once, yea twice, though man does not regard it.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falls upon men, in slumberings upon the bed.
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Then he opens the ears of men, and seals their instruction
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
that he may withdraw man from his purpose, and hide pride from man.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
He keeps back his soul from the pit, and his life from perishing by the sword.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
He also is chastened with pain upon his bed, and with continual strife in his bones,
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
so that his life abhors bread, and his soul dainty food.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
His flesh is consumed away that it cannot be seen. And his bones that were not seen stick out.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Yea, his soul draws near to the pit, and his life to the destroyers.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
If there be with him an agent, an interpreter, one among a thousand, to show to man what is right for him,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
then God is gracious to him, and says, Deliver him from going down to the pit; I have found a ransom.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
His flesh shall be fresher than a child's. He returns to the days of his youth.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
He prays to God, and he is favorable to him, so that he sees his face with joy, and he restores to man his righteousness.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
He sings before men, and says, I have sinned, and perverted that which was right, and it did not profit me.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He has redeemed my soul from going into the pit, and my life shall behold the light.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Lo, all these things God works twice, yea thrice, with a man,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
to bring back his soul from the pit, that he may be enlightened with the light of the living.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Mark well, O Job, hearken to me. Keep silent, and I will speak.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
If thou have anything to say, answer me. Speak, for I desire to justify thee.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
If not, hearken thou to me. Keep silent, and I will teach thee.

< Ayubu 33 >