< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Slyšiž tedy, prosím, Jobe, řeči mé, a všech slov mých ušima svýma pozoruj.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Aj, jižť otvírám ústa svá, mluví jazyk můj v ústech mých.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Upřímost srdce mého a umění vynesou rtové moji.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
Duch Boha silného učinil mne, a dchnutí Všemohoucího dalo mi život.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Můžeš-li, odpovídej mi, připrav se proti mně, a postav se.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Aj, já podlé žádosti tvé buduť místo Boha silného; z bláta sformován jsem i já.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Pročež strach ze mne nepředěsí tě, a ruka má nebudeť k obtížení.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Řekl jsi pak přede mnou, a hlas ten řečí tvých slyšel jsem:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
Čist jsem, bez přestoupení, nevinný jsem, a nepravosti při mně není.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Aj, příčiny ku potření mne shledal Bůh, klade mne sobě za nepřítele,
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
Svírá poutami nohy mé, střeže všech stezek mých.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Aj, tím nejsi spravedliv, odpovídám tobě, nebo větší jest Bůh nežli člověk.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Oč se s ním nesnadníš? Žeť všech svých věcí nezjevuje?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
Ano jednou mluví Bůh silný, i dvakrát, a nešetří toho člověk.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
Skrze sny u vidění nočním, když připadá hluboký sen na lidi ve spaní na ložci,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
Tehdáž odkrývá ucho lidem, a čemu je učí, to zpečeťuje,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
Aby odtrhl člověka od skutku zlého, a pýchu od muže vzdálil,
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
A zachoval duši jeho od jámy, a život jeho aby netrefil na meč.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
Tresce i bolestí na lůži jeho, a všecky kosti jeho násilnou nemocí,
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
Tak že sobě život jeho oškliví pokrm, a duše jeho krmi nejlahodnější.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Hyne tělo jeho patrně, a vyhlédají kosti jeho, jichž prvé nebylo vídati.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
A tak bývá blízká hrobu duše jeho, a život jeho smrtelných ran.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
Však bude-li míti anděla vykladače jednoho z tisíce, kterýž by za člověka oznámil pokání jeho:
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
Tedy smiluje se nad ním, a dí: Vyprosť jej, ať nesstoupí do porušení, oblíbilť jsem mzdu vyplacení.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
I odmladne tělo jeho nad dítěcí, a navrátí se ke dnům mladosti své.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
Kořiti se bude Bohu, a zamiluje jej, a patřiti bude na něj tváří ochotnou; nadto navrátí člověku spravedlnost jeho.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
Kterýž hledě na lidi, řekne: Zhřešilť jsem byl, a to, což pravého bylo, převrátil jsem, ale nebylo mi to prospěšné.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
Bůh však vykoupil duši mou, aby nešla do jámy, a život můj, aby světlo spatřoval.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Aj, všeckoť to dělá Bůh silný dvakrát i třikrát při člověku,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
Aby odvrátil duši jeho od jámy, a aby osvícen byl světlem živých.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Pozoruj, Jobe, poslouchej mne, mlč, ať já mluvím.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Jestliže máš slova, odpovídej mi, nebo bych chtěl ospravedlniti tebe.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Pakli nic, ty mne poslouchej; mlč, a poučím tě moudrosti.

< Ayubu 33 >