< Ayubu 32 >

1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
Então aquelles tres homens cessaram de responder a Job; porque era justo aos seus proprios olhos.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
E accendeu-se a ira d'Elihu, filho de Baracheel o buzita, da familia de Ram: contra Job se accendeu a sua ira, porque se justificava a si mesmo, mais do que a Deus.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Tambem a sua ira se accendeu contra os seus tres amigos: porque, não achando que responder, todavia condemnavam a Job.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Elihu porém esperou que Job fallasse; porquanto tinham mais edade do que elle.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
Vendo pois Elihu que já não havia resposta na bocca d'aquelles tres homens, a sua ira se accendeu.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
E respondeu Elihu, filho de Baracheel o buzita, e disse: Eu sou de menos edade, e vós sois edosos; receei-me e temi de vos declarar a minha opinião.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
Dizia eu: Fallem os dias, e a multidão doa annos ensine a sabedoria.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Na verdade, ha um espirito no homem, e a inspiração do Todo-poderoso os faz entendidos.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Os grandes não são os sabios, nem os velhos entendem juizo.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Pelo que digo: Dae-me ouvidos, e tambem eu declararei a minha opinião.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Eis que aguardei as vossas palavras, e dei ouvidos ás vossas considerações, até que buscasseis razões.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Attentando pois para vós, eis que nenhum de vós ha que possa convencer a Job, nem que responda ás suas razões:
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Para que não digaes: Achamos a sabedoria; Deus o derribou, e não homem algum.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Ora elle não dirigiu contra mim palavra alguma, nem lhe responderei com as vossas palavras.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Estão pasmados, não respondem mais, faltam-lhes as palavras.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
Esperei pois, porém não fallam: porque já pararam, e não respondem mais.
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Tambem eu responderei pela minha parte: tambem eu declararei a minha opinião.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
Porque estou cheio de palavras, e aperta-me o espirito do meu ventre.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Eis que o meu ventre é como o mosto, sem respiradouro, e virá a arrebentar, como odres novos.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Fallarei, e respirarei: abrirei os meus labios, e responderei.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Oxalá eu não faça accepção de pessoas, nem use de sobrenomes com o homem!
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Porque não sei usar de sobrenomes: em breve me levaria o meu Creador.

< Ayubu 32 >