< Ayubu 32 >
1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
Tad tie trīs vīri mitējās Ījabam atbildēt, tāpēc ka tas pats sevi turēja par taisnu.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Bet Elihus, Baraheēļa dēls, tas Buzietis, no Rāma radiem, apskaitās pret Ījabu lielās dusmās, tāpēc ka tas savu dvēseli taisnoja pār Dievu.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Viņš arī apskaitās par saviem trim draugiem, ka tie atbildes neatrada un tomēr Ījabu pazudināja.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Jo Elihus bija gaidījis ar Ījabu runāt, tāpēc ka tie bija vecāki nekā viņš.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
Bet kad Elihus redzēja, ka atbildes nebija to triju vīru mutē, tad viņš apskaitās.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
Un Elihus, Baraheēļa dēls, tas Buzietis, atbildēja un sacīja: es esmu jauns, bet jūs esat veci, tāpēc es esmu gaidījis un bijājies, jums izteikt savu padomu.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
Es domāju: lai tie gadi runā, un gadu vairums lai izteic gudrību.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Bet tas ir Tas Gars iekš cilvēka un tā visuvarenā Dieva dvaša, kas tos dara gudrus.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Veci nav tie gudrākie nedz sirmgalvji, kas prot tiesu.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Tādēļ es gribu runāt, - klausiet mani, es arīdzan parādīšu savu zināšanu.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Redzi, es esmu gaidījis uz jūsu vārdiem, esmu klausījies uz jūsu gudrību, vai jūs atrastu tos īstenos vārdus.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Kad es nu jūs liku vērā, redzi, tad nav neviena, kas Ījabu būtu pārliecinājis, kas uz viņa vārdiem būtu atbildējis jūsu starpā.
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Tad nu nesakāt: mēs esam dzirdējuši gudrību; Dievs vien viņu pārvarēs, un ne cilvēks.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Pret mani vēl viņš vārda nav cēlis, un ar jūsu valodu es viņam gan neatbildēšu. -
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Tie ir izbiedēti, vairs nevar atbildēt, tiem trūkst valodas.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
Es esmu gaidījis, bet tie nerunā, tie stāv klusu un vairs neatbild.
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Tad nu es atbildēšu savu tiesu, es arīdzan parādīšu savu zināšanu.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
Jo es esmu tik pilns vārdu, ka gars manu sirdi spiež.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Redzi, mana sirds ir kā jauns vīns, kas nestāv vaļā, tā gribētu plīst, kā jauni ādas trauki.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Es runāšu, lai es varu atpūsties, es atdarīšu savas lūpas un atbildēšu.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Cilvēka vaigu es neuzlūkošu un nerunāšu nevienam pa prātam.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Jo cilvēkam pa prātam runāt es nemāku, lai mans Radītājs mani ātri neaizņem projām.