< Ayubu 32 >

1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
Alors ces trois hommes cessèrent de répondre à Job, parce qu’il se croyait toujours juste.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Mais Eliu, fils de Barachel, le Buzite, de la famille de Ram, s’irrita et s’indigna; or il s’irrita contre Job, de ce qu’il disait qu’il était juste devant Dieu.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Puis il s’indigna contre ses amis, de ce qu’ils n’avaient pas trouvé de réponse raisonnable contre Job, mais que seulement ils l’avaient condamné.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Ainsi Eliu attendit tant que Job parla, parce que ceux qui parlèrent étaient plus âgés que lui.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
Mais lorsqu’il eut vu que les trois n’avaient pu répondre, il fut vivement irrité.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
Répondant donc, Eliu, fils de Barachel, le Buzite, dit: Je suis le plus jeune, et vous, vous êtes plus âgés, c’est pourquoi, la tête baissée, je n’ai pas osé manifester mon sentiment.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
Car j’espérais qu’un âge aussi avancé parlerait, et qu’une multitude d’années enseignerait la sagesse.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Mais, comme je le vois, l’Esprit est dans les hommes et l’inspiration du Tout-Puissant donne l’intelligence.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Ce ne sont pas ceux qui ont vécu longtemps qui sont sages, et ce ne sont pas les vieillards qui comprennent la justice.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
C’est pourquoi je parlerai: Ecoutez-moi, je vous montrerai, moi aussi, ma sagesse.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Car j’ai attendu vos discours; j’ai écouté pour voir quelle était votre prudence, tant que vous avez fait assaut de discours.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Et tant que je pensais que vous diriez quelque chose, j’étais attentif; mais, comme je le vois, il n’y a personne de vous qui puisse convaincre Job et répondre à ses discours.
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
N’allez pas dire: Nous avons trouvé la sagesse; Dieu l’a rejeté et non un homme.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Il ne m’a rien dit, et pour moi, ce ne sera pas selon vos discours que je lui répondrai.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Ils ont été épouvantés, ils n’ont plus répondu, ils se sont ôté à eux-mêmes la parole.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
Puisque donc j’ai attendu, et qu’ils n’ont point parlé; qu’ils se sont arrêtés, et qu’ils n’ont plus répondu,
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Je parlerai moi aussi pour ma part, et je montrerai ma science.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
Car je suis plein de discours, et une force me presse au dedans de moi.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Voilà que mon estomac est comme un vin nouveau qui, sans air, rompt les outres neuves,
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Je parlerai et je respirerai un peu; j’ouvrirai mes lèvres.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Je ne ferai acception de personne, et je n’égalerai pas Dieu à un homme.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Car je ne sais combien de temps je subsisterai, et si dans peu mon Créateur ne m’enlèvera point.

< Ayubu 32 >