< Ayubu 32 >

1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
Ces trois hommes cessèrent donc de répondre à Job, car il était juste à ses propres yeux.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Alors la colère d'Élihu, fils de Barachel, le Buzite, de la famille de Ram, s'enflamma contre Job. Sa colère s'enflamma parce qu'il se justifiait lui-même plutôt que Dieu.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Sa colère s'enflamma aussi contre ses trois amis, parce qu'ils n'avaient pas trouvé de réponse, et qu'ils avaient pourtant condamné Job.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Or Élihu avait attendu pour parler à Job, car ils étaient plus âgés que lui.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
Quand Élihu vit qu'il n'y avait pas de réponse dans la bouche de ces trois hommes, sa colère s'enflamma.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
Elihu, fils de Barachel, le Buzite, répondit, « Je suis jeune, et vous êtes très vieux. C'est pourquoi je me suis retenu, et je n'ai pas osé te montrer mon opinion.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
J'ai dit: « Les jours doivent parler, et la multitude d'années devrait enseigner la sagesse.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Mais il y a un esprit dans l'homme, et l'Esprit du Tout-Puissant leur donne l'intelligence.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Ce ne sont pas les grands qui sont sages, ni les personnes âgées qui comprennent la justice.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
C'est pourquoi j'ai dit: « Écoutez-moi; Je vais aussi montrer mon opinion.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
« Voici, j'attendais tes paroles, et j'ai écouté votre raisonnement, pendant que tu cherchais quoi dire.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Oui, je vous ai accordé toute mon attention, mais personne n'a convaincu Job, ou qui ont répondu à ses paroles, parmi vous.
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Prenez garde de ne pas dire: « Nous avons trouvé la sagesse ». Dieu peut le réfuter, pas l'homme;
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
car il n'a pas dirigé ses paroles contre moi; je ne lui répondrai pas non plus par vos discours.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
« Ils sont stupéfaits. Ils ne répondent plus. Ils n'ont pas un mot à dire.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
Dois-je attendre, car ils ne parlent pas? parce qu'ils restent immobiles, et ne répondent plus?
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Je vais aussi répondre à ma part, et je vais aussi montrer mon opinion.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
Car je suis plein de paroles. L'esprit qui est en moi me contraint.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Voici, ma poitrine est comme un vin qui n'a pas d'issue; comme des outres neuves, il est prêt à éclater.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Je vais parler, pour me rafraîchir. Je vais ouvrir mes lèvres et répondre.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
S'il vous plaît, ne me laissez pas respecter la personne d'un homme, Je ne donnerai pas non plus de titres flatteurs à un homme.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Car je ne sais pas donner des titres flatteurs, ou bien mon Créateur m'emporterait bientôt.

< Ayubu 32 >