< Ayubu 32 >
1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
Forsothe these thre men leften of to answere Joob, for he semyde a iust man to hem.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
And Helyu, the sone of Barachel Buzites, of the kynrede of Ram, was wrooth, and hadde indignacioun; forsothe he was wrooth ayens Joob, for he seide hym silf to be iust bifor God.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Sotheli Helyu hadde indignacioun ayens the thre frendis of hym, for thei hadden not founde resonable answere, but oneli hadde condempned Joob.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Therfor Helyu abood Joob spekynge, for thei, that spaken, weren eldere men.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
But whanne he hadde seyn, that thre men myyten not answere, he was wrooth greetly.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
And Helyu, the sone of Barachel Buzites, answeride, and seyde, Y am yongere in tyme, sotheli ye ben eldere; therfor with heed holdun doun Y dredde to schewe to you my sentence.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
For Y hopide that lengere age schulde speke, and that the multitude of yeeris schulden teche wisdom.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
But as Y se, spirit is in men, and the enspiryng `ether reuelacioun, of Almyyti God yyueth vndurstondyng.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Men of long lijf ben not wise, and elde men vndurstonden not doom.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Therfor Y schal seie, Here ye me, and Y also schal schewe my kunnyng to you.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
For Y abood youre wordis, Y herde youre prudence, as long as ye dispuytiden in youre wordis.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
And as long as Y gesside you to seie ony thing, Y bihelde; but as Y se, `noon is of you, that may repreue Joob, and answere to hise wordis;
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
lest perauenture ye seien, We han founde wisdom; God, and not man, hath cast hym awei.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Joob spak no thing to me, and Y not bi youre wordis schal answere hym.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Thei dredden, and answeriden no more, and token awei speche fro hem silf.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
Therfor for Y abood, and thei spaken not, thei stoden, and answeriden no more; also Y schal answere my part,
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
and Y schal schewe my kunnyng.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
For Y am ful of wordis, and the spirit of my wombe, `that is, mynde, constreyneth me.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Lo! my wombe is as must with out `spigot, ether a ventyng, that brekith newe vessels.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Y schal speke, and brethe ayen a litil; Y schal opene my lippis, and Y schal answere.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Y schal not take the persoone of man, and Y schal not make God euene to man.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
For Y woot not hou long Y schal abide, and if my Makere take me awei `after a litil tyme.