< Ayubu 32 >

1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
So these three men ceased to answere Iob, because he esteemed himselfe iust.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Then the wrath of Elihu the sonne of Barachel the Buzite, of the familie of Ram, was kindled: his wrath, I say, was kindled against Iob, because he iustified himselfe more then God.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Also his anger was kindled against his three friends, because they could not finde an answere, and yet condemned Iob.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
(Now Elihu had wayted til Iob had spoken: for they were more ancient in yeeres then he)
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
So when Elihu saw, that there was none answere in the mouth of the three men, his wrath was kindled.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
Therefore Elihu the sonne of Barachel, the Buzite answered, and sayd, I am yong in yeres, and ye are ancient: therefore I doubted, and was afraide to shewe you mine opinion.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
For I said, The dayes shall speake, and the multitude of yeeres shall teach wisedome.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Surely there is a spirite in man, but the inspiration of the Almightie giueth vnderstanding.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Great men are not alway wise, neither doe the aged alway vnderstand iudgement.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Therefore I say, Heare me, and I will shew also mine opinion.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Behold, I did waite vpon your wordes, and hearkened vnto your knowledge, whiles you sought out reasons.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Yea, when I had considered you, lo, there was none of you that reproued Iob, nor answered his wordes:
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Lest ye should say, We haue found wisedome: for God hath cast him downe, and no man.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Yet hath he not directed his words to me, neyther will I answere him by your wordes.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Then they fearing, answered no more, but left off their talke.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
When I had wayted (for they spake not, but stood still and answered no more)
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Then answered I in my turne, and I shewed mine opinion.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
For I am full of matter, and the spirite within me compelleth me.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Beholde, my belly is as the wine, which hath no vent, and like the new bottels that brast.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Therefore will I speake, that I may take breath: I will open my lippes, and will answere.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
I will not now accept the person of man, neyther will I giue titles to man.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
For I may not giue titles, lest my Maker should take me away suddenly.

< Ayubu 32 >