< Ayubu 32 >
1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
And his three friends also ceased any longer to answer Job: for Job was righteous before them.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Then Elius the son of Barachiel, the Buzite, of the kindred of Ram, of the country of Ausis, was angered: and he was very angry with Job, because he justified himself before the Lord.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
And he was also very angry with [his] three friends, because they were not able to return answers to Job, yet set him down for an ungodly man.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
But Elius had forborne to give an answer to Job, because they were older than he.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
And Elius saw that there was no answer in the mouth of the three men; and he was angered in his wrath.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
And Elius the Buzite the son of Barachiel answered and said, I am younger in age, and you are elder, therefore I kept silence, fearing to declare to you my own knowledge.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
And I said, It is not time that speaks, though in many years [men] know wisdom:
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
but there is a spirit in mortals; and the inspiration of the Almighty is that which teaches.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
The long-lived are not wise [as such]; neither do the aged know judgement.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Therefore I said, Hear me, and I will tell you what I know.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Listen to my words; for I will speak in your hearing, until you shall have tried [the matter] with words:
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
and I shall understand as far as you; and, behold, there was no one of you that answered Job his words in argument,
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
lest you should say, We have found that we have added wisdom to the Lord.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
And you have commissioned a man to speak such words.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
They were afraid, they answered no longer; they gave up their speaking.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
I waited, (for I had not spoken, ) because they stood still, they answered not.
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
And Elius continued, and said, I will again speak,
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
for I am full of words, for the spirit of my belly destroys me.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
And my belly is as a skin of sweet wine, bound up [and] ready to burst; or as a brazier's labouring bellows.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
I will speak, that I may open my lips and relieve myself.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
For truly I will not be awed because of man, nor indeed will I be confounded before a mortal.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
For I know not how to respect persons: and if otherwise, even the moths would eat me.