< Ayubu 32 >
1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
因為約伯自以為義,那三個友人就不再回答他。
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
那時,有個布次蘭族的人,他是巴辣革耳的兒子厄里烏,為了約伯在天主前自以為義人,便大為憤怒;
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
同時也對約伯的三個友人大為震怒,因為他們找不到適當的答覆,又以天主為不公。
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
厄里烏先等他們同約伯講完話,因為他們都比他年老。
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
他一見他們三人無話可說:遂大為憤怒。
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
於是布次人巴辣革耳的兒子厄里烏發言說:我年齡小,你們年紀大,故此我退縮畏懼,不敢在你們前表示我的見解。
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
我心想:「老人應先發言,年高者應教人智慧。」
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
但人本來都具有靈性,全能者的氣息賦與人聰明;
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
並不是年高者就有智慧,老年人就通曉正義。
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
故此我請你們且聽我說,我也要表示我的見解。
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
直到如今,我等待你們講話,靜聽你們的理論,等待你們尋出適當的言詞;
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
但現今我已明白看出了,你們中沒一個能駁倒約伯,能回答他的話的。
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
你們不要說:「我們尋到了智慧! 只有天主可說服他,人卻不能。」
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
我決不那樣辯論,也決不以你們說的話答覆他。
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
他們已心亂,不能再回答,且已窮於辭令。
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
他們已不再講話了,他們已停止,不再答話了,我還等什麼﹖
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
現在我要開始講我的一段話,表示出我的見解。
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
因為我覺著充滿了要說的話,內心催迫著我。
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
看啊! 我內心像尋覓出口的新酒,要將新酒囊爆裂。
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
我一說出,必覺輕鬆,我定要開口發言。
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
我決不顧情面,也決不奉承人。
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
因為我不會奉承,不然,造我者必立即將我消滅。