< Ayubu 32 >

1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
И така, тия трима човека престанаха да отговарят на Иова, защото беше праведен пред своите си очи.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Тогава пламна гневът на вузеца Елиу, син на Варахиила, от Арамовото семейство. Гневът му пламна против Иова, защото оправдаваше себе си наместо Бога
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
тоже против тримата му приятели пламна гневът му, защото бяха осъдили Иова без да му намерят отговор.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
А Елиу беше чакал да говори на Иова, защото другите бяха по-стари от него.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
Но когато Елиу видя, че нямаше отговор в устата на тия трима мъже, гневът му пламна.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
Тогава вузецът Елиу, син на Варахиила, в отговор рече: - Аз съм млад, а вие много стари; Затова се посвених, и не смеех да ви явя моето мнение.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
Аз рекох: Дните нека говорят, И многото години нека учат мъдрост.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
Но има дух в човека; Вдъхновението на Всемогъщия го вразумява.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Не че човеците са велики, за това ще са и мъдри, Нито че са стари, за това ще разбират правосъдието.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Прочее, казвам: Слушайте мене; Нека явя и аз мнението си.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Ето, чаках докато вие говорехте, Слушах разсъжденията ви, Когато търсехте какво да кажете;
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Внимателно ви слушах, И ето, ни един от вас не убеди Иова, Нито отговори на думите му;
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
За да не речете: Ние намерихме мъдрост. Бог ще го свали, а не човек.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Понеже той не е отправил думите си против мене, То и аз няма да му отговоря според вашите речи.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
Те се смайват, не отговарят вече, Не намират ни дума да кажат.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
А да чакам ли аз понеже те не говорят, - Понеже стоят и не отговарят вече?
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
Нека отговоря и аз от моя страна, Нека явя и аз мнението си.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
Защото съм пълен с думи; Духът в мене дълбоко ме притиска.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Ето коремът ми е като вино неотворено, Близо е да се разпукне като нови мехове.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
Ще проговоря, за да ми стане по-леко; Ще отворя устните си и ще отговоря.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Далеч от мене да гледам на лице, Или да полаская човека.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Защото не зная да лаская; Иначе Създателят ми би ме отмахнал веднага.

< Ayubu 32 >