< Ayubu 31 >
1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
“Me prometí a mí mismo no mirar nunca con deseo a las jóvenes.
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
¿Qué debe esperar la gente de Dios? ¿Qué recompensa debe darles el Todopoderoso en lo alto?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
¿No es el desastre para los malvados y la destrucción para los que hacen el mal?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
¿No ve Dios todo lo que hago, incluso cuenta cada paso que doy?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
¿He vivido una vida engañosa? ¿He estado ansioso por decir mentiras?
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
¡No! Que Dios me pese en la balanza de su justicia y que descubra mi integridad.
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
“Si me he desviado del camino de Dios, si he dejado que lo que veo se convierta en mis deseos, si hay alguna mancha de pecado en mis manos,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
entonces que otro coma lo que he sembrado, y que todo lo que he cultivado sea desarraigado.
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Si una mujer me ha seducido, o si he buscado la oportunidad de acostarme con la mujer de mi prójimo,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
que mi esposa sirva a otro, que otros hombres se acuesten con ella.
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Porque eso sería una maldad, un pecado que merece castigo,
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
porque este pecado es como un fuego que lleva a la destrucción, destruyendo todo lo que tengo.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
“Si me negara a escuchar a mis siervos o siervas cuando me trajeran sus quejas,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
¿qué haría cuando Dios viniera a juzgarme? ¿Cómo respondería si me investigara?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
¿Acaso el mismo Dios no nos hizo a todos?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
¿Me he negado a dar a los pobres lo que necesitaban, o he hecho desesperar a las viudas?
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
¿Acaso he comido yo solo un trozo de pan? ¿No he compartido siempre mi comida con los huérfanos?
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
Desde que era joven fui padre de los huérfanos y cuidé de las viudas.
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
Si alguna vez veía a alguien necesitado de ropa, a los pobres sin nada que ponerse,
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
siempre me agradecían la ropa de lana que los mantenía calientes.
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
“Si levantaba la mano para golpear a un huérfano, seguro de que si llegaba a los tribunales los jueces estarían de mi parte,
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
entonces que mi hombro sea arrancado de su articulación, que mi brazo sea arrancado de su cavidad.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Como me aterra el castigo que Dios me tiene reservado, y debido a su majestad, nunca podría hacer esto.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
“¿He puesto mi confianza en el oro, llamando al oro fino ‘mi seguridad’?
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
¿Me he deleitado en ser rico, feliz por todas mis riquezas que había ganado?
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
¿He mirado el sol brillando tan intensamente o la luna moviéndose con majestuosidad por el cielo
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
y he tenido la tentación de adorarlos secretamente besando mi mano ante ellos como señal de devoción?
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
Esto también sería un pecado que merece castigo porque significaría que he negado a Dios en lo alto.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
“¿Alguna vez me he alegrado cuando el desastre destruyó a los que me odiaban, o he celebrado cuando el mal los derribó?
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
Nunca he permitido que mi boca pecara echando una maldición sobre la vida de alguien.
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
¿No ha preguntado mi familia: ‘¿Hay alguien que no haya comido todo lo que quería de su comida?’
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
Nunca he dejado dormir a extraños en la calle; he abierto mis puertas a los viajeros.
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
¿He ocultado mis pecados a los demás, escondiendo mi maldad en lo más profundo de mí?
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
¿Tenía miedo de lo que pensaran los demás, del desprecio que me hicieran las familias, y por eso me callaba y no salía?
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
“¿Por qué nadie escucha lo que digo? Firmo con mi nombre para avalar todo lo que he dicho. Que el Todopoderoso me responda. Que mi acusador escriba de qué me acusa.
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Yo los pondría en alto; Los llevaría en mi cabeza como una corona.
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Le explicaría todo lo que había hecho; mantendría la cabeza alta ante él.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
“Si mi tierra ha gritado contra mí; si sus surcos han llorado por mí;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
si he tomado sus cosechas sin pago o si he causado daño a los agricultores;
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
entonces que crezcan espinas en lugar de trigo, y cizaña en lugar de cebada”. Las palabras de Job se terminan.