< Ayubu 31 >
1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
Eu fiz um pacto com meus olhos; como, pois, eu olharia com cobiça para a virgem?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Pois qual é a porção [dada] por Deus acima, e a herança [dada] pelo Todo-Poderoso das alturas?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
Por acaso a calamidade não é para o perverso, e o desastre para os que praticam injustiça?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Por acaso ele não vê meus caminhos, e conta todos os meus passos?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
Se eu andei com falsidade, e se meu pé se apressou para o engano,
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
Pese-me ele em balanças justas, e Deus saberá minha integridade.
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
Se meus passos se desviaram do caminho, e meu coração seguiu meus olhos, e se algo se apegou às minhas mãos,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
Que eu semeie, e outro coma; e meus produtos sejam arrancados.
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Se foi meu coração se deixou seduzir por [alguma] mulher, ou se estive espreitei à porta de meu próximo,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
Que minha mulher moa para outro, e outros se encurvem sobre ela.
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Pois tal seria um crime vergonhoso, e delito [a ser sentenciado por] juízes.
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
Pois seria um fogo que consumiria até à perdição, e destruiria toda a minha renda.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
Se desprezei o direito de meu servo ou de minha serva quando eles reclamaram comigo,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
Que faria eu quando Deus se levantasse? E quando ele investigasse [a causa], o que eu lhe responderia?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Aquele que me fez no ventre [materno também] não fez a ele? E não nos preparou de um mesmo [modo] na madre?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
Se eu neguei aos pobres o que eles desejavam, ou fiz desfalecer os olhos da viúva;
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
E se comi meu alimento sozinho, e o órfão não comeu dele
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
(Porque desde a minha juventude cresceu comigo como [se eu fosse seu pai], e desde o ventre de minha mãe guiei [a viúva] );
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
Se eu vi alguém morrer por falta de roupa, e o necessitado sem algo que o cobrisse,
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
Se sua cintura não me bendisse, quando ele se esquentava com as peles de meus cordeiros;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
Se levantei minha mão contra o órfão, quando vi que seria favorecido na corte judicial,
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
Que minha escápula caia do meu ombro, e meu braço se quebre de sua articulação.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Porque o castigo de Deus era um assombro para mim, e eu não teria poder contra sua majestade.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
Se eu pus no ouro minha esperança, ou disse ao ouro fino: Tu és minha confiança;
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
Se eu me alegrei de que minha riqueza era muita, e de que minha mão havia obtido muito;
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
Se olhei para o sol quando brilhava, e à lua quando estava bela,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
E meu coração se deixou enganar em segredo, e minha boca beijou minha mão,
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
Isto também seria um delito [a ser sentenciado por] juiz; porque teria negado ao Deus de cima.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
Se eu me alegrei da desgraça daquele que me odiava, e me agradei quando o mal o encontrou,
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
Sendo que nem deixei minha boca pecar, desejando sua morte com maldição,
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
Se a gente da minha casa nunca tivesse dito: Quem não se satisfez da carne dada por ele?
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
O estrangeiro não passava a noite na rua; eu abria minhas portas ao viajante.
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
Se encobri minhas transgressões como as pessoas [fazem], escondendo meu delito em meu seio;
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
Porque eu tinha medo da grande multidão, e o desprezo das famílias me atemorizou; então me calei, e não saí da porta:
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Quem me dera se alguém me ouvisse! Eis que minha vontade é que o Todo-Poderoso me responda, e meu adversário escrevesse um relato da acusação.
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Certamente eu o carregaria sobre meu ombro, e o poria em mim como uma coroa.
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Eu lhe diria o número de meus passos, e como um príncipe eu me chegaria a ele.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Se minha terra clamar contra mim, e seus sulcos juntamente chorarem;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
Se comi seus frutos sem [pagar] dinheiro, ou fiz expirar a alma de seus donos;
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
Em lugar de trigo que [me] produza cardos, e ervas daninhas no lugar da cevada. [Aqui] terminam as palavras de Jó.