< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
Pepigi fœdus cum oculis meis ut ne cogitarem quidem de virgine.
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Quam enim partem haberet in me Deus desuper, et hereditatem Omnipotens de excelsis?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
Numquid non perditio est iniquo, et alienatio operantibus iniustitiam?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Nonne ipse considerat vias meas, et cunctos gressus meos dinumerat?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
Si ambulavi in vanitate, et festinavit in dolo pes meus:
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
Appendat me in statera iusta, et sciat Deus simplicitatem meam.
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
Si declinavit gressus meus de via, et si secutum est oculos meos cor meum, et si manibus meis adhæsit macula:
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
Seram, et alium comedat: et progenies mea eradicetur.
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Si deceptum est cor meum super muliere, et si ad ostium amici mei insidiatus sum:
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
Scortum alterius sit uxor mea, et super illam incurventur alii.
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Hoc enim nefas est, et iniquitas maxima.
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
Ignis est usque ad perditionem devorans, et omnia eradicans genimina.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
Si contempsi subire iudicium cum servo meo, et ancilla mea, cum disceptarent adversum me:
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
Quid enim faciam cum surrexerit ad iudicandum Deus? et cum quæsierit, quid respondebo illi?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Numquid non in utero fecit me qui et illum operatus est: et formavit me in vulva unus?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
Si negavi, quod volebant, pauperibus, et oculos viduæ expectare feci:
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
Si comedi buccellam meam solus, et non comedit pupillus ex ea:
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
(Quia ab infantia mea crevit mecum miseratio: et de utero matris meæ egressa est mecum.)
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
Si despexi pereuntem, eo quod non habuerit indumentum, et absque operimento pauperem:
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
Si non benedixerunt mihi latera eius, et de velleribus ovium mearum calefactus est:
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
Si levavi super pupillum manum meam, etiam cum viderem me in porta superiorem:
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
Humerus meus a iunctura sua cadat, et brachium meum cum suis ossibus confringatur.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Semper enim quasi tumentes super me fluctus timui Deum, et pondus eius ferre non potui.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
Si putavi aurum robur meum, et obrizo dixi: Fiducia mea.
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
Si lætatus sum super multis divitiis meis, et quia plurima reperit manus mea.
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
Si vidi solem cum fulgeret, et lunam incedentem clare:
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
Et lætatum est in abscondito cor meum, et osculatus sum manum meam ore meo.
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
Quæ est iniquitas maxima, et negatio contra Deum altissimum.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
Si gavisus sum ad ruinam eius, qui me oderat, et exultavi quod invenisset eum malum.
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
Non enim dedi ad peccandum guttur meum, ut expeterem maledicens animam eius.
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
Si non dixerunt viri tabernaculi mei: Quis det de carnibus eius ut saturemur:
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
Foris non mansit peregrinus, ostium meum viatori patuit.
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
Si abscondi quasi homo peccatum meum, et celavi in sinu meo iniquitatem meam.
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
Si expavi ad multitudinem nimiam, et despectio propinquorum terruit me: et non magis tacui, nec egressus sum ostium.
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Quis mihi tribuat auditorem, ut desiderium meum audiat Omnipotens: et librum scribat ipse qui iudicat.
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Ut in humero meo portem illum, et circumdem illum quasi coronam mihi?
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Per singulos gradus meos pronunciabo illum, et quasi principi offeram eum.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Si adversum me terra mea clamat, et cum ipsa sulci eius deflent:
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
Si fructus eius comedi absque pecunia, et animam agricolarum eius afflixi:
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
Pro frumento oriatur mihi tribulus, et pro hordeo spina. (Finita sunt verba Iob.)

< Ayubu 31 >