< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
Io avevo stretto un patto con gli occhi miei; come dunque avrei fissati gli sguardi sopra una vergine?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Che parte mi avrebbe assegnata Iddio dall’alto e quale eredità m’avrebbe data l’Onnipotente dai luoghi eccelsi?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
La sventura non è ella per il perverso e le sciagure per quelli che fanno il male?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Iddio non vede egli le mie vie? non conta tutti i miei passi?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
Se ho camminato insieme alla menzogna, se il piede mio s’è affrettato dietro alla frode
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
(Iddio mi pesi con bilancia giusta e riconoscerà la mia integrità)
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
se i miei passi sono usciti dalla retta via, se il mio cuore è ito dietro ai miei occhi, se qualche sozzura mi s’è attaccata alle mani,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
ch’io semini e un altro mangi, e quel ch’è cresciuto nei miei campi sia sradicato!
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Se il mio cuore s’è lasciato sedurre per amor d’una donna, se ho spiato la porta del mio prossimo,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
che mia moglie giri la macina ad un altro, e che altri abusino di lei!
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Poiché quella è una scelleratezza, un misfatto punito dai giudici,
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
un fuoco che consuma fino a perdizione, e che avrebbe distrutto fin dalle radici ogni mia fortuna.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
Se ho disconosciuto il diritto del mio servo e della mia serva, quand’eran meco in lite,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
che farei quando Iddio si levasse per giudicarmi, e che risponderei quando mi esaminasse?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Chi fece me nel seno di mia madre non fece anche lui? non ci ha formati nel seno materno uno stesso Iddio?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
Se ho rifiutato ai poveri quel che desideravano, se ho fatto languire gli occhi della vedova,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
se ho mangiato da solo il mio pezzo di pane senza che l’orfano ne mangiasse la sua parte,
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
io che fin da giovane l’ho allevato come un padre, io che fin dal seno di mia madre sono stato guida alla vedova,
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
se ho visto uno perire per mancanza di vesti o il povero senza una coperta,
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
se non m’hanno benedetto i suoi fianchi, ed egli non s’è riscaldato colla lana dei miei agnelli,
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
se ho levato la mano contro l’orfano perché mi sapevo sostenuto alla porta…
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
che la mia spalla si stacchi dalla sua giuntura, il mio braccio si spezzi e cada!
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
E invero mi spaventava il castigo di Dio, ed ero trattenuto dalla maestà di lui.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
Se ho riposto la mia fiducia nell’oro, se all’oro fino ho detto: “Tu sei la mia speranza”,
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
se mi son rallegrato che le mie ricchezze fosser grandi e la mia mano avesse molto accumulato,
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
se, contemplando il sole che raggiava e la luna che procedeva lucente nel suo corso,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
il mio cuore, in segreto, s’è lasciato sedurre e la mia bocca ha posato un bacio sulla mano
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
(misfatto anche questo punito dai giudici ché avrei difatti rinnegato l’Iddio ch’è di sopra),
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
se mi son rallegrato della sciagura del mio nemico ed ho esultato quando gli ha incolto sventura
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
(io, che non ho permesso alle mie labbra di peccare chiedendo la sua morte con imprecazione),
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
se la gente della mia tenda non ha detto: “Chi è che non si sia saziato della carne delle sue bestie?”
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
(lo straniero non passava la notte fuori; le mie porte erano aperte al viandante),
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
se, come fan gli uomini, ho coperto i miei falli celando nel petto la mia iniquità,
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
perché avevo paura della folla e dello sprezzo delle famiglie al punto da starmene queto e non uscir di casa…
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Oh, avessi pure chi m’ascoltasse!… ecco qua la mia firma! l’Onnipotente mi risponda! Scriva l’avversario mio la sua querela,
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
ed io la porterò attaccata alla mia spalla, me la cingerò come un diadema!
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Gli renderò conto di tutt’i miei passi, a lui m’appresserò come un principe!
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Se la mia terra mi grida contro, se tutti i suoi solchi piangono,
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
se ne ho mangiato il frutto senza pagarla, se ho fatto sospirare chi la coltivava,
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
che invece di grano mi nascano spine, invece d’orzo mi crescano zizzanie!” Qui finiscono i discorsi di Giobbe.

< Ayubu 31 >