< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
J'avais fait un accord avec mes yeux; et comment aurais-je regardé une vierge?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Car quelle part Dieu m'aurait-il faite d'en haut, et quel héritage le Tout-Puissant m'aurait-il envoyé des cieux?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
La calamité n'est-elle pas pour le pervers, et l'adversité pour ceux qui commettent l'iniquité?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Ne voit-il pas toute ma conduite, et ne compte-t-il pas tous mes pas?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
Si j'ai marché dans le mensonge, et si mon pied s'est hâté pour tromper,
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
Que Dieu me pèse dans des balances justes, et il reconnaîtra mon intégrité.
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
Si mes pas se sont détournés de la voie, et si mon cœur a suivi mes yeux, et si quelque souillure s'est attachée à mes mains,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
Que je sème et qu'un autre mange, et que mes rejetons soient déracinés!
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Si mon cœur a été séduit par quelque femme, et si j'ai fait le guet à la porte de mon prochain,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
Que ma femme broie le grain pour un autre, et que d'autres se penchent sur elle!
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Car c'est là une méchanceté préméditée, une iniquité punie par les juges.
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
C'est un feu qui dévore jusqu'à pleine destruction, qui eût ruiné tous mes biens dans leur racine.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
Si j'ai méprisé le droit de mon serviteur ou de ma servante, quand ils ont eu des contestations avec moi,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
Et que ferais-je, quand Dieu se lèvera, et quand il demandera compte, que lui répondrais-je?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Celui qui m'a fait dans le sein de ma mère, ne l'a-t-il pas fait aussi? Un même créateur ne nous a-t-il pas formés dans le sein maternel?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
Si j'ai refusé aux pauvres leur demande, si j'ai laissé se consumer les yeux de la veuve,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
Si j'ai mangé seul mon morceau, et si l'orphelin n'en a point mangé,
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
Certes, dès ma jeunesse, il a grandi près de moi comme près d'un père, et dès le sein de ma mère, j'ai été le guide de la veuve,
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
Si j'ai vu un homme périr faute de vêtement, et le pauvre manquer de couverture;
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
Si ses reins ne m'ont pas béni, et s'il n'a pas été réchauffé par la toison de mes agneaux;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
Si j'ai levé ma main contre l'orphelin, parce que je me voyais appuyé à la porte;
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
Que mon épaule tombe de ma nuque, et que mon bras soit cassé et séparé de l'os!
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Car la frayeur serait sur moi avec la calamité de Dieu, et je ne pourrais pas subsister devant sa majesté.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
Si j'ai mis dans l'or ma confiance, et si j'ai dit à l'or fin: Tu es ma sécurité;
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
Si je me suis réjoui de ce que ma fortune était grande, et de ce que ma main avait beaucoup acquis;
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
Si, voyant le soleil briller et la lune s'avancer magnifique,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
Mon cœur a été secrètement séduit, et si ma main a envoyé des baisers
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
(Ce qui est aussi une iniquité punie par le juge, car c'est un reniement du Dieu d'en haut);
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
Si je me suis réjoui du malheur de mon ennemi, si j'ai sauté de joie quand le mal l'a atteint
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
(Je n'ai pas permis à ma langue de pécher en demandant sa mort dans des malédictions);
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
Si les gens de ma maison n'ont pas dit: “Où y a-t-il quelqu'un qui n'ait été rassasié de sa viande? “
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
(L'étranger ne passait pas la nuit dehors; j'ouvrais ma porte au voyageur);
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
Si j'ai caché, comme Adam, mes fautes; si j'ai enfermé mon crime dans mon sein,
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
Parce que je craignais la foule et redoutais le mépris des familles, en sorte que je restais tranquille et n'osais franchir ma porte.
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Oh! si quelqu'un m'écoutait! Voici ma signature: Que le Tout-Puissant me réponde, et que mon adversaire écrive son mémoire!
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Je jure que je le porterai sur mon épaule, je me l'attacherai comme une couronne,
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Je lui déclarerai le nombre de mes pas, je l'aborderai comme un prince.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Si ma terre crie contre moi, et si mes sillons pleurent avec elle;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
Si je mange ses fruits sans l'avoir payée, si je fais rendre l'âme à ses maîtres,
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
Qu'elle produise de l'épine au lieu de froment, et l'ivraie au lieu d'orge! C'est ici la fin des paroles de Job.

< Ayubu 31 >