< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
J'avais fait accord avec mes yeux; comment aurais-je donc arrêté mes regards sur une vierge?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Et quelle [serait] la portion [que] Dieu [m'aurait envoyée] d'en haut, et quel eût été l'héritage que le Tout-puissant m'eût [envoyé] des hauts lieux?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
La perdition n'est-elle pas pour l'injuste, et les accidents étranges pour les ouvriers d'iniquité?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
N'a-t-il pas vu lui-même mes voies, et n'a-t-il pas compté toutes mes démarches?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
Si j'ai marché dans le mensonge, et si mon pied s'est hâté à tromper,
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
Qu'on me pèse dans des balances justes, et Dieu connaîtra mon intégrité.
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
Si mes pas se sont détournés du [droit] chemin, et si mon cœur a marché après mes yeux, et si quelque tache s'est attachée à mes mains,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
Que je sème, et qu'un autre mange [ce que j'aurai semé]; et que tout ce que j'aurai fait produire, soit déraciné!
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Si mon cœur a été séduit après quelque femme, et si j'ai demeuré en embûche à la porte de mon prochain,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
Que ma femme soit déshonorée par un autre, et qu'elle soit prostituée à d'autres!
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Vu que c'est une méchanceté préméditée, une de ces iniquités qui sont toutes jugées.
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
Car c'est un feu qui dévore jusqu'à consumer, et qui aurait déraciné tout mon revenu.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
Si j'ai refusé de faire droit à mon serviteur ou à ma servante, quand ils ont contesté avec moi;
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
Car qu'eussé-je fait, quand le [Dieu] Fort se fût levé? et quand il m'en eût demandé compte, que lui aurais-je répondu?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Celui qui m'a formé dans le ventre, ne les a-t-il pas faits aussi? et ne nous a-t-il pas tous formés de la même manière dans la matrice?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
Si j'ai refusé aux pauvres ce qu'ils ont désiré; si j'ai fait consumer les yeux de la veuve;
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
Si j'ai mangé seul mes morceaux, et si l'orphelin n'en a point mangé;
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
(Car dès ma jeunesse il a été élevé avec moi, comme [chez son père], et dès le ventre de ma mère j'ai conduit l'orphelin.)
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
Si j'ai vu un homme périr faute d'être vêtu, et le pauvre faute de couverture;
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
Si ses reins ne m'ont point béni, et s'il n'a pas été échauffé de la laine de mes agneaux;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
Si j'ai levé la main contre l'orphelin, quand j'ai vu à la porte, que je pouvais l'aider;
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
Que l'os de mon épaule tombe et que mon bras soit cassé, et séparé de l'os auquel il est joint!
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Car j'ai eu frayeur de l'orage du [Dieu] Fort, et je ne saurais [subsister] devant sa majesté.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
Si j'ai mis mon espérance en l'or, et si j'ai dit au fin or: Tu es ma confiance;
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
Si je me suis réjoui de ce que mes biens étaient multipliés, et de ce que ma main en avait trouvé abondamment;
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
Si j'ai regardé le soleil lorsqu'il brillait le plus, et la lune marchant noblement;
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
Et si mon cœur a été séduit en secret, et si ma main a baisé ma bouche;
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
(Ce qui est aussi une iniquité toute jugée; car j'eusse renié le Dieu d'en haut.)
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
Si je me suis réjoui du malheur de celui qui me haïssait; si j'ai sauté de joie quand il lui est arrivé du mal.
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
Je n'ai pas même permis à ma langue de pécher, en demandant sa mort avec imprécation.
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
Et les gens de ma maison n'ont point dit: Qui nous donnera de sa chair? nous n'en saurions être rassasiés.
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
L'étranger n'a point passé la nuit dehors; j'ai ouvert ma porte au passant.
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
Si j'ai caché mon péché comme Adam, pour couvrir mon iniquité en me flattant.
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
Quoique je pusse me faire craindre à une grande multitude, toutefois le moindre qui fût dans les familles m'inspirait de la crainte, et je me tenais dans le silence, et ne sortais point de la porte.
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Ô! s'il y avait quelqu'un qui voulût m'entendre. Tout mon désir est que le Tout-puissant me réponde, et que ma partie adverse fasse un écrit [contre moi].
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Si je ne le porte sur mon épaule, et si je ne l'attache comme une couronne.
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Je lui raconterais tous mes pas, je m'approcherais de lui comme d'un Prince.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Si ma terre crie contre moi, et si ses sillons pleurent;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
Si j'ai mangé son fruit sans argent; si j'ai tourmenté l'esprit de ceux qui la possédaient.
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
Qu'elle me produise des épines au lieu de blé, et de l'ivraie au lieu d'orge. C'est ici la fin des paroles de Job.

< Ayubu 31 >