< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
J’avais fait un pacte avec mes yeux, et comment aurais-je arrêté mes regards sur une vierge. —
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
Quelle part, me disais-je, Dieu me réserverait-il d’en haut? Quel sort le Tout-Puissant me ferait-il de son ciel?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
La ruine n’est-elle pas pour le méchant, et le malheur pour les artisans d’iniquité?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Dieu ne connaît-il pas mes voies, ne compte-t-il pas tous mes pas?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
Si j’ai marché dans le sentier du mensonge, si mon pied a couru après la fraude, —
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
que Dieu me pèse dans de justes balances, et il reconnaîtra mon innocence!
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
Si mes pas se sont écartés du droit chemin, si mon cœur a suivi mes yeux, si quelque souillure s’est attachée à mes mains, —
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
que je sème, et qu’un autre mange, que mes rejetons soient déracinés!
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Si mon cœur a été séduit par une femme, si j’ai fait le guet à la porte de mon prochain, —
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
que ma femme tourne la meule pour un autre, que des étrangers la déshonorent!
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Car c’est là un crime horrible, un forfait que punissent les juges;
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
un feu qui dévore jusqu’à la ruine, qui aurait détruit tous mes biens.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
Si j’ai méconnu le droit de mon serviteur ou de ma servante, quand ils étaient en contestation avec moi: —
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
Que faire, quand Dieu se lèvera? Au jour de sa visite, que lui répondrai-je?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Celui qui m’a fait dans le sein de ma mère ne l’a-t-il pas fait aussi? Un même Créateur ne nous a-t-il pas formés?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
Si j’ai refusé aux pauvres ce qu’ils désiraient, si j’ai fait languir les yeux de la veuve,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
si j’ai mangé seul mon morceau de pain, sans que l’orphelin en ait eu sa part: —
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
dès mon enfance il m’a gardé comme un père; dès ma naissance il a guidé mes pas.
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
Si j’ai vu le malheureux périr sans vêtements, l’indigent manquer de couverture,
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
sans que ses reins m’aient béni, sans que la toison de mes agneaux l’ait réchauffé;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
si j’ai levé la main contre l’orphelin, parce que je me voyais un appui dans les juges, —
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
que mon épaule se détache du tronc, que mon bras soit arraché de l’humérus.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Car je crains la vengeance de Dieu, et devant sa majesté je ne puis subsister.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
Si j’ai mis dans l’or mon assurance, si j’ai dit à l’or pur: « Tu es mon espoir; »
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
si je me suis réjoui de l’abondance de mes biens, des trésors amassés par mes mains;
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
si, en voyant le soleil jeter ses feux, et la lune s’avancer dans sa splendeur,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
mon cœur s’est laissé séduire en secret, si ma main s’est portée à ma bouche, —
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
c’est là encore un crime que punit le juge; j’aurais renié le Dieu très-haut.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
Si j’ai été joyeux de la ruine de mon ennemi, si j’ai tressailli d’allégresse quand le malheur l’a frappé: —
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
Non, je n’ai pas permis à ma langue de pécher, en demandant sa mort avec imprécation!...
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
Si les gens de ma tente ne disaient pas: « Où trouver quelqu’un qui ne soit pas rassasiés de sa table? »
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
si l’étranger passait la nuit en dehors, si je n’ouvrais pas la porte au voyageur!...
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
Si j’ai, comme font les hommes, déguisé mes fautes, et renfermé mes iniquités dans mon sein,
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
par peur de la grande assemblée, par crainte du mépris des familles, au point de me taire, et de n’oser franchir le seuil de ma porte!...
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Oh! Qui me fera trouver quelqu’un qui m’écoute? Voilà ma signature: que le Tout-Puissant me réponde! Que mon adversaire écrive aussi sa cédule!
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
On verra si je ne la mets pas sur mon épaule, si je n’en ceins pas mon front comme d’un diadème!
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
Je rendrai compte à mon juge de tous mes pas, je m’approcherai de lui comme un prince.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Si ma terre crie contre moi, si j’ai fait pleurer ses sillons;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
si j’ai mangé ses produits sans l’avoir payée, si je l’ai arrachée à ses légitimes possesseurs, —
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
qu’au lieu de froment il y naisse des épines, et de l’ivraie au lieu d’orge! Ici finissent les discours de Job.

< Ayubu 31 >