< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
I made a couenant with mine eyes: why then should I thinke on a mayde?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
For what portion should I haue of God from aboue? and what inheritance of the Almightie from on hie?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
Is not destruction to the wicked and strange punishment to the workers of iniquitie?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Doeth not he beholde my wayes and tell all my steps?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
If I haue walked in vanitie, or if my foote hath made haste to deceite,
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
Let God weigh me in the iust balance, and he shall know mine vprightnes.
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
If my steppe hath turned out of the way, or mine heart hath walked after mine eye, or if any blot hath cleaued to mine handes,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
Let me sowe, and let another eate: yea, let my plantes be rooted out.
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
If mine heart hath bene deceiued by a woman, or if I haue layde wayte at the doore of my neighbour,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
Let my wife grinde vnto another man, and let other men bow downe vpon her:
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
For this is a wickednes, and iniquitie to bee condemned:
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
Yea, this is a fire that shall deuoure to destruction, and which shall roote out al mine increase,
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
If I did contemne the iudgement of my seruant, and of my mayde, when they did contend with me,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
What then shall I do when God standeth vp? and when he shall visit me, what shall I answere?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
He that hath made me in the wombe, hath he not made him? hath not he alone facioned vs in the wombe?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
If I restrained the poore of their desire, or haue caused the eyes of the widow to faile,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
Or haue eaten my morsels alone, and the fatherles hath not eaten thereof,
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
(For from my youth hee hath growen vp with me as with a father, and from my mothers wombe I haue bene a guide vnto her)
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
If I haue seene any perish for want of clothing, or any poore without couering,
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
If his loynes haue not blessed me, because he was warmed with the fleece of my sheepe,
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
If I haue lift vp mine hande against the fatherlesse, when I saw that I might helpe him in the gate,
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
Let mine arme fal from my shoulder, and mine arme be broken from the bone.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
For Gods punishment was fearefull vnto me, and I could not be deliuered from his highnes.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
If I made gold mine hope, or haue sayd to the wedge of golde, Thou art my confidence,
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
If I reioyced because my substance was great, or because mine hand had gotten much,
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
If I did behold the sunne, when it shined, or the moone, walking in her brightnes,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
If mine heart did flatter me in secrete, or if my mouth did kisse mine hand,
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
(This also had bene an iniquitie to be condemned: for I had denied the God aboue)
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
If I reioyced at his destruction that hated me, or was mooued to ioye when euill came vpon him,
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
Neither haue I suffred my mouth to sinne, by wishing a curse vnto his soule.
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
Did not the men of my Tabernacle say, Who shall giue vs of his flesh? we can not bee satisfied.
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
The stranger did not lodge in the streete, but I opened my doores vnto him, that went by the way.
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
If I haue hid my sinne, as Adam, concealing mine iniquitie in my bosome,
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
Though I could haue made afraid a great multitude, yet the most contemptible of the families did feare me: so I kept silence, and went not out of the doore.
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Oh that I had some to heare me! beholde my signe that the Almightie will witnesse for me: though mine aduersary should write a booke against me,
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Woulde not I take it vpon my shoulder, and binde it as a crowne vnto me?
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
I will tell him the nomber of my goings, and goe vnto him as to a prince.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
If my lande cry against me, or the furrowes thereof complayne together,
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
If I haue eaten the fruites thereof without siluer: or if I haue grieued the soules of the masters thereof,
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
Let thistles growe in steade of wheate, and cockle in the stead of Barley. The wordes of Iob are ended.

< Ayubu 31 >