< Ayubu 31 >
1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
I made a covenant with mine eyes; and how should I fix my regard upon a maid?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
For what would have been [my] portion of God from above, and what the heritage of the Almighty from on high?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
Is not calamity for the unrighteous? and misfortune for the workers of iniquity?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Doth not he see my ways, and number all my steps?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
If I have walked with falsehood, and my foot hath hasted to deceit,
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
(Let me be weighed in an even balance, and God will take knowledge of my blamelessness; )
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
If my step have turned out of the way, and my heart followed mine eyes, and if any blot cleaveth to my hands;
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
Let me sow, and another eat; and let mine offspring be rooted out.
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
If my heart have been enticed unto a woman, so that I laid wait at my neighbour's door,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
Let my wife grind for another, and let others bow down upon her.
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
For this is an infamy; yea, it is an iniquity [to be judged by] the judges:
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
For it is a fire that consumeth to destruction, and would root out all mine increase.
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
If I have despised the cause of my bondman or of my bondmaid, when they contended with me,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
What then should I do when God riseth up? and if he visited, what should I answer him?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Did not he that made me in the womb make him? and did not One fashion us in the womb?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
If I have withheld the poor from [their] desire, or caused the eyes of the widow to fail;
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
Or have eaten my morsel alone, so that the fatherless ate not thereof,
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
(For from my youth he grew up with me as with a father, and I have guided the [widow] from my mother's womb; )
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
If I have seen any perishing for want of clothing, or any needy without covering;
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
If his loins have not blessed me, and if he were not warmed with the fleece of my lambs;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
If I have lifted up my hand against an orphan, because I saw my help in the gate:
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
[Then] let my shoulder fall from the shoulder-blade, and mine arm be broken from the bone!
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
For calamity from God was a terror to me, and by reason of his excellency I was powerless.
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
If I have made gold my hope, or said to the fine gold, My confidence!
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
If I rejoiced because my wealth was great, and because my hand had gotten much;
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
If I beheld the sun when it shone, or the moon walking in brightness,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
And my heart have been secretly enticed, so that my mouth kissed my hand:
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
This also would be an iniquity for the judge, for I should have denied the God who is above.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
If I rejoiced at the destruction of him that hated me, and exulted when evil befell him;
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
(Neither have I suffered my mouth to sin by asking his life with a curse; )
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
If the men of my tent said not, Who shall find one that hath not been satisfied with his meat? —
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
The stranger did not lodge without; I opened my doors to the pathway.
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
If I covered my transgressions as Adam, by hiding mine iniquity in my bosom,
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
Because I feared the great multitude, and the contempt of families terrified me, so that I kept silence, and went not out of the door, ...
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Oh that I had one to hear me! Behold my signature: let the Almighty answer me! And let mine opponent write an accusation!
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Would I not take it upon my shoulder? I would bind it on to me [as] a crown;
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
I would declare unto him the number of my steps; as a prince would I come near to him.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
If my land cry out against me, and its furrows weep together;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
If I have eaten the fruits thereof without money, and have tormented to death the souls of its owners:
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
Let thistles grow instead of wheat, and tares instead of barley. The words of Job are ended.