< Ayubu 31 >

1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
Jeg sluttede en Pagt med mit Øje om ikke at se paa en Jomfru;
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
hvad var ellers min Lod fra Gud hist oppe, den Arv, den Almægtige gav fra det høje?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
Har ikke den lovløse Vanheld i Vente, Udaadsmændene Modgang?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
Ser han ej mine Veje og tæller alle mine Skridt?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
Har jeg holdt til med Løgn, og hasted min Fod til Svig —
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
paa Rettens Vægtskaal veje han mig, saa Gud kan kende min Uskyld —
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
er mit Skridt bøjet af fra Vejen, og har mit Hjerte fulgt mine Øjne, hang noget ved mine Hænder,
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
da gid jeg maa saa og en anden fortære, og hvad jeg planted, oprykkes med Rode!
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
Blev jeg en Daare paa Grund af en Kvinde, og har jeg luret ved Næstens Dør,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
saa dreje min Hustru Kværn for en anden, og andre bøje sig over hende!
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Thi sligt var Skændselsdaad, Brøde, der drages for Retten,
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
ja, Ild, der æder til Afgrunden og sætter hele min Høst i Brand!
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
Har jeg ringeagtet min Træls og min Trælkvindes Ret, naar de trættede med mig,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
hvad skulde jeg da gøre, naar Gud stod op, hvad skulde jeg svare, naar han saa efter?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
Har ikke min Skaber skabt ham i Moders Skød, har en og samme ej dannet os begge i Moders Liv?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
Har jeg afslaaet ringes Ønske, ladet Enkens Øjne vansmægte,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
var jeg ene om at spise mit Brød, har den faderløse ej spist deraf —
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
nej, fra Barnsben fostred jeg ham som en Fader, jeg ledede hende fra min Moders Skød.
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
Har jeg set en Stakkel blottet for Klæder, en fattig savne et Tæppe —
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
visselig nej, hans Hofter velsigned mig, naar han varmed sig i Uld af mine Lam.
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
Har jeg løftet min Baand mod en faderløs, fordi jeg var vis paa Medhold i Retten,
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
saa falde min Skulder fra Nakken, saa rykkes min Arm af Led!
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
Thi Guds Rædsel var kommet over mig, og naar han rejste sig, magted jeg intet!
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
Har jeg slaaet min Lid til Guld, kaldt det rene Guld min Fortrøstning,
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
var det min Glæde, at Rigdommen voksed, og at min Haand fik sanket saa meget,
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
saa jeg, hvorledes Sollyset straaled, eller den herligt skridende Maane,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
og lod mit Hjerte sig daare i Løn, saa jeg hylded dem med Kys paa min Haand —
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
ogsaa det var Brøde, der drages for Retten, thi da fornægted jeg Gud hist oppe.
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
Var min Avindsmands Fald min Glæd jubled jeg, naar han ramtes af Vanheld —
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
nej, jeg tillod ikke min Gane at synde, saa jeg bandende kræved hans Sjæl.
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
Har min Husfælle ej maattet sige: »Hvem mættedes ej af Kød fra hans Bord« —
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
nej, den fremmede laa ej ude om Natten, jeg aabned min Dør for Vandringsmænd.
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
Har jeg skjult mine Synder, som Mennesker gør, saa jeg dulgte min Brøde i Brystet
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
af Frygt for den store Hob, af Angst for Stamfrænders Ringeagt, saa jeg blev inden Døre i Stilhed! —
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
Ak, var der dog en, der hørte paa mig! Her er mit Bomærke — lad den Almægtige svare! Havde jeg blot min Modparts Indlæg!
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
Sandelig, tog jeg det paa min Skulder, kransed mit Hoved dermed som en Krone,
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
svared ham for hvert eneste Skridt og mødte ham som en Fyrste.
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
Har min Mark maattet skrige over mig og alle Furerne græde,
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
har jeg tæret dens Kraft uden Vederlag, udslukt dens Ejeres Liv,
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
saa gro der Tjørn for Hvede og Ukrudt i Stedet for Byg! Her ender Jobs Ord.

< Ayubu 31 >