< Ayubu 31 >
1 “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
我與眼睛立約, 怎能戀戀瞻望處女呢?
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
從至上的上帝所得之分, 從至高全能者所得之業是甚麼呢?
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
豈不是禍患臨到不義的, 災害臨到作孽的呢?
4 Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
上帝豈不是察看我的道路, 數點我的腳步呢?
5 “Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
我若與虛謊同行, 腳若追隨詭詐; (
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
我若被公道的天平稱度, 使上帝可以知道我的純正;)
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
我的腳步若偏離正路, 我的心若隨着我的眼目, 若有玷污粘在我手上;
8 basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
就願我所種的有別人吃, 我田所產的被拔出來。
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
我若受迷惑,向婦人起淫念, 在鄰舍的門外蹲伏,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
就願我的妻子給別人推磨, 別人也與她同室。
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
因為這是大罪, 是審判官當罰的罪孽。
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
這本是火焚燒,直到毀滅, 必拔除我所有的家產。
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
我的僕婢與我爭辯的時候, 我若藐視不聽他們的情節;
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
上帝興起,我怎樣行呢? 他察問,我怎樣回答呢?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
造我在腹中的,不也是造他嗎? 將他與我摶在腹中的豈不是一位嗎?
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
我若不容貧寒人得其所願, 或叫寡婦眼中失望,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
或獨自吃我一點食物, 孤兒沒有與我同吃; (
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
從幼年時孤兒與我同長,好像父子一樣; 我從出母腹就扶助 寡婦。)
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
我若見人因無衣死亡, 或見窮乏人身無遮蓋;
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
我若不使他因我羊的毛得暖, 為我祝福;
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
我若在城門口見有幫助我的, 舉手攻擊孤兒;
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
情願我的肩頭從缺盆骨脫落, 我的膀臂從羊矢骨折斷。
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
因上帝降的災禍使我恐懼; 因他的威嚴,我不能妄為。
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
我若以黃金為指望, 對精金說:你是我的倚靠;
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
我若因財物豐裕, 因我手多得資財而歡喜;
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
我若見太陽發光, 明月行在空中,
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
心就暗暗被引誘, 口便親手;
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
這也是審判官當罰的罪孽, 又是我背棄在上的上帝。
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
我若見恨我的遭報就歡喜, 見他遭災便高興; (
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
我沒有容口犯罪, 咒詛他的生命;)
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
若我帳棚的人未嘗說, 誰不以主人的食物吃飽呢? (
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
從來我沒有容客旅在街上住宿, 卻開門迎接行路的人;)
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
我若像亞當 遮掩我的過犯, 將罪孽藏在懷中;
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
因懼怕大眾, 又因宗族藐視我使我驚恐, 以致閉口無言,杜門不出;
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
惟願有一位肯聽我! (看哪,在這裏有我所劃的押, 願全能者回答我!)
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
願那敵我者所寫的狀詞在我這裏! 我必帶在肩上,又綁在頭上為冠冕。
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
我必向他述說我腳步的數目, 必如君王進到他面前。
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
我若奪取田地,這地向我喊冤, 犂溝一同哭泣;
39 kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
我若吃地的出產不給價值, 或叫原主喪命;
40 basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.
願這地長蒺藜代替麥子, 長惡草代替大麥。 約伯的話說完了。