< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
Pero ahora se ríen de mí personas mucho más jóvenes que yo; personas a cuyos padres no pondría a trabajar con mis perros pastores.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Son demasiado débiles para serme útiles y están agotados.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Adelgazados por el hambre y la necesidad, tratan de comer la tierra seca en el desierto oscuro y desolado.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Allí recogen hierbas del desierto y las hojas de los arbustos, y comen las raíces de las retamas.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
Fueron expulsados de la comunidad.
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
La gente gritaba tras ellos como si fueran ladrones. Tienen que vivir en barrancos peligrosos, en cuevas y entre las rocas.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Gritan como animales entre los arbustos; se acurrucan entre la maleza para refugiarse.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
Son gente insensata, sin nombre, que ha sido expulsada de la tierra.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
Pero ahora se burlan de mí en sus cantos; ¡me he convertido en un chiste para ellos!
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Me desprecian y rehúyen; no dudan en escupirme a la cara.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Dios ha aflojado la cuerda de mi arco y me ha humillado.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
La chusma se levanta contra mí, y me hace correr; como una ciudad sitiada planifican formas de destruirme.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Cortan mi vía de escape; provocan mi caída y lo hacen sin ayuda de nadie.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Entran por una amplia brecha; se precipitan mientras el muro se derrumba.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Me invaden los terrores; mi honor se lo lleva el viento; mi salvación se desvanece como una nube.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
Y ahora mi vida se desvanece; cada día la desesperación me atenaza.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
Por la noche mis huesos agonizan; el dolor me roe y no cesa.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Dios me agarra bruscamente por la ropa; me tira del cuello de la camisa.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Me ha arrojado al barro; me ha humillado como polvo y ceniza.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Dios, clamo a ti, pero no respondes; me presento ante ti, pero ni siquiera te fijas en mí.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Te has vuelto cruel conmigo; usas tu poder para hacerme sufrir.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Me levantas y me llevas en el viento; me arrojas en el torbellino.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Sé que me llevas a la muerte, al lugar donde van todos los vivos.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
¿Quién querría dar una patada a un hombre cuando está abatido, cuando claman por ayuda en su momento de dificultad?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
¿No lloré por los que pasaban por momentos difíciles? ¿No me afligí por lo que sufrían los pobres?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
Pero cuando busqué el bien, sólo vino el mal, y cuando esperé la luz, todo lo que vino fue oscuridad.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
En mi interior hay confusión, nunca se detiene; me enfrento a días de desesperación.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Estoy tan deprimido; ver el sol no ayuda. Me pongo de pie en la asamblea y clamo por ayuda.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Soy como un hermano de los chacales, un compañero de los búhos.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Mi piel se ennegrece sobre mí; y mis huesos arden dentro de mí.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Mi lira sólo toca canciones tristes, y mi pipa es la voz de los que lloran.

< Ayubu 30 >