< Ayubu 30 >
1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
“Mas ahora se ríen de mí los que tienen menos años que yo, a cuyos padres yo hubiera desdeñado de tomar como perros para mi ganado.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Aun la fuerza de sus manos ¿de qué me habría servido? ya que carecen ellos de todo vigor.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Muertos de miseria y de hambre roen el yermo, la tierra desolada y vacía.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Recogen frutos amargos de arbustos, y se sustentan con raíces de retama.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
Expulsados de la sociedad, y perseguidos con gritos habitan como ladrones,
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
en los barrancos de los torrentes, en las cuevas de la tierra y en las breñas.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Entre la maleza lanzan sus gritos, y se reúnen bajo las zarzas.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
Son hombres insensatos, hijos de gente sin nombre, echados del país a viva fuerza.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
Y ahora soy escarnecido por ellos y el objeto de sus pullas.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Me abominan, se apartan de mí; y no se avergüenzan de escupirme en la cara.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Han perdido todo freno, me humillan y pierden todo respeto en mi presencia.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
A mi derecha se levanta el populacho; hacen vacilar mis pies; traman contra mí maquinaciones para perderme.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Me cortan el camino, procuran mi caída; nadie me presta auxilio contra ellos.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Como por brecha ancha irrumpen, se revuelcan entre los escombros.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Me han acometido terrores, y como el viento se llevan mi nobleza; cual nube pasó mi prosperidad.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
Ahora mi vida se derrama dentro de mí, se han apoderado de mí días aciagos.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
La noche me taladra los huesos, y no me dan tregua los que me roen.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Su gran muchedumbre ha desfigurado mi vestido; me ciñen como el cabezón de mi túnica.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Me han echado en el lodo, soy como el polvo y la ceniza.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
A Ti clamo por auxilio, y Tú no me respondes; permanezco en pie, y Tú me miras (con indiferencia).
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Te has tornado para mí en enemigo, y me persigues con todo tu poder.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Me alzas sobre el viento, y me haces cabalgar; me sacudes sin darme sostén.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Porque bien sé que me entregarás a la muerte, a la casa adonde van a parar todos los vivientes.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Sin embargo el que va a perecer ¿no extiende su mano? en su aflicción ¿no pide auxilio?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
¿No lloraba yo con el atribulado? ¿no se afligía mi alma por el pobre?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
Pero esperando el bien, me vino el mal; aguardando la luz he quedado cubierto de tinieblas.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Mis entrañas se abrazan sin descanso; me han sobrevenido días de aflicción.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Ando como quien está de luto, sin alegría, me levanto en la asamblea para clamar por auxilio.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Soy ahora hermano de los chacales, y compañero de los avestruces.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Ennegrecida se me cae la piel, y mis huesos se consumen por la fiebre.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
El son de mi cítara se ha trocado en lamentos, y mi flauta en voz de llanto.”